Senegal, ambayo imemaliza ya tatu katika Kundi la I siku ya Ijumaa, Juni 26, ni miongoni mwa timu nane bora kutinga kufikia hatua hii na hivyo imejihakikishia nafasi yake katika hatua ya 16 bora ya michuano ya Kombe la Dunia la 2026, kutokana na matokeo ya Kundi G.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Senegal ilinufaika na sare ya Iran dhidi ya Misri (1-1) na ushindi mkubwa wa Ubelgiji dhidi ya New Zealand (5-1). Lakini pia ni kutokana na ushindi wake mkubwa dhidi ya Iraq (5-0), ambao unaipa jumla ya pointi 3 na tofauti kubwa ya mabao ya +2, bora kuliko ile ya timu zilizoshika nafasi ya tatu katika Kundi A (Korea Kusini, pointi 3, -1), C (Scotland, pointi 3, -3), G (Iran, pointi 3, 0), na H (Uruguay, pointi 2, -1).
Wakati huo huo Cape Verde wametoka sare na Saudi Arabia, na hivyo kutinga hatua ya 16 bora huku Uhispania ikiongoza kundi.
Cape Verde walipata sare ya tatu mfululizo dhidi ya Saudi Arabia (0-0) mnamo Juni 26 huko Houston, lakini pia kufanikiwa kutinga hatua ya 16 bora kwa mara ya kwanza kabisa kwa hatua ya mtoano ya Kombe la Dunia, wakisaidiwa na kichapo cha Uruguay dhidi ya Uhispania (0-1). Blue Sharks walimaliza wa pili katika Kundi H (alama 3) nyuma ya La Roja na watakabiliana na Argentina katika hatua ya 16 bora.