- Ajali ya uso kwa uso kati ya lori na gari aina ya Nissan imeua waigizaji wawili wa Kenya na kuwapeleka wengine 12 hospitalini
- Waigizaji hao walikuwa wakielekea Mombasa kwa ajili ya onyesho la setbook wakati lori lilipopoteza mwelekeo na kuligonga gari lao
- Walionusurika wanaomba msaada wa kifedha ili kugharamia matibabu, huku mwigizaji mmoja wa Kenya akisimulia yaliyotokea katika mahojiano ya kipekee na TUKO.co.ke
Waigizaji wawili wa Kenya wamefariki dunia huku wengine 12 wakipokea matibabu hospitalini kufuatia ajali ya uso kwa uso iliyotokea wakati kundi hilo lilipokuwa likielekea Mombasa kwa ajili ya onyesho la setbook.

Source: UGC
Katika mahojiano ya kipekee na TUKO.co.ke, mwigizaji Tony Sherman alifichua tukio hilo, akisema watu wote 14 waliokuwa kwenye gari walikuwa waigizaji wa setbook na filamu waliokuwa wamemaliza onyesho moja na walikuwa wakielekea lingine Mombasa ajali ilipotokea.
“Inasemekana ilihappen jana saa saba mchana, and they were from a show wakielekea ingine yenye ilikua ifanywe Mombasa,” Sherman alisema.
Nini kilisababisha ajali hiyo?
Chanzo cha pili chenye ufahamu wa tukio hilo kilisema lori lilipoteza mwelekeo na kugongana uso kwa uso na matatu iliyokuwa imewabeba waigizaji hao.
“Ilikuwa ajali ya uso kwa uso kati ya lori na Nissan yao. Lori lilipoteza mwelekeo na kuwagonga. Wawili walifariki na wengine wakakimbizwa hospitalini,” chanzo hicho kilisema.
Ajali hiyo inaripotiwa kutokea majira ya saa 1:00 jioni.
Baada ya ajali hiyo, waigizaji waliojeruhiwa walipelekwa katika hospitali mbalimbali kwa matibabu.
Walionusurika waomba msaada wa kifedha
Sherman aliomba umma kuwasaidia kifedha, akibainisha kuwa waigizaji waliolazwa hospitalini wanahitaji fedha zaidi ili kupata matibabu yanayostahili.
Wanaotaka kuchangia wanaweza kutuma msaada kupitia Pochi La Biashara kwa nambari 0726310658, iliyosajiliwa kwa jina la Mary Olalo.

Source: UGC
Wakenya waliwapa pole waigizaji hao vijana na kuandika jumbe za kugusa moyo kwa heshima ya wawili waliofariki.
Ajali nyingine katika Barabara ya Nairobi-Mombasa
Katika habari nyingine, pia tuliangazia taarifa kuhusu ajali mbaya iliyotokea kwenye Barabara Kuu ya Nairobi-Mombasa, iliyosababisha vifo vya watu sita huku wengine saba wakijeruhiwa.

Pia soma
“Tuliponea chupuchupu”: Familia ya Kakamega yasimulia dakika za kutisha baada ya ajali ya Tahmeed
Uchunguzi bado unaendelea huku mamlaka zikijaribu kubaini kilichosababisha ajali hiyo mbaya iliyohusisha basi la abiria na malori mawili.
Tukio hilo ni ukumbusho mkubwa wa hatari za ajali za barabarani, hasa nyakati za usiku.
Wakati wahudumu wa dharura waliendelea kufanya kazi bila kuchoka kuwaokoa walionusurika, jamii zimeendelea kuomboleza waliopoteza maisha huku zikitoa wito wa kuimarishwa kwa usalama barabarani.
Read: ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.
Chanzo: TUKO.co.ke
