Marufuku ya uagizaji na biashara ya dhahabu kutoka Sudan imetangazwa siku ya Jumatatu, Julai 13, 2026, katika jaribio la kupunguza vyanzo vya ufadhili kwa mzozo wa Sudan. Mzozo huu ni kati ya jeshi la serikali na vikosi vya wanamgambo wa RSF kwa zaidi ya miaka mitatu. Hatua hii ya Umoja wa Ulaya pia inapiga marufuku uuzaji na uhamisho wa zebaki na sianidi kwenda Sudan, vitu vinavyotumika katika uchimbaji wa dhahabu.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

“Dhahabu imekuwa chanzo kikuu cha mapato kinachochochea mzozo nchini Sudan,” linasema Baraza la Umoja wa Ulaya.

Sudan ni mojawapo ya wazalishaji wakubwa wa dhahabu barani Afrika. Na akiba yake ni chanzo kikubwa cha mapato kwa pande zote mbili zinazopigana. Vikosi vyawanamgambo vinadhibiti migodi ya dhahabu katika maeneo ya Darfur na Kordofan, huku jeshi la Sudan likidhibiti yale yaliyo mashariki na kaskazini.

Mwaka wa 2024, kwa kila tani 31 za dhahabu iliyosafirishwa kihalali, wataalam wanakadiria kuwa tani 40 zilisafirishwa nje ya nchi kimagendo. Dhahabu hiyo husafirishwa hasa kupitia nchi jirani—Misri, Chad, na Libya—kabla ya kufika Dubai katika Falme za Kiarabu, kitovu cha kimataifa cha kusafisha na kufanya biashara ya dhahabu.

Wataalamu wanaonya kwamba vikwazo hivi vya Umoja wa Ulaya pekee havitatosha kuzuia ufadhili wa vita. Umoja wa Ulaya huagiza chini ya 10% ya dhahabu iliyouzwa duniani.

Zaidi ya hayo, 90% ya dhahabu inayosafirishwa kutoka Sudan husafirishwa kupitia Dubai, ambapo hakuna utaratibu wa ufuatiliaji wa chuma hiki cha thamani. Hata kiasi kidogo cha dhahabu kilichonunuliwa na nchi wanachama wa EU hakiwezi kufuatiliwa hadi Sudan.

Kulingana na mtafiti Cameron Hudson, vikwazo hivi vya Ulaya ni vya kiishara tu. Ili kuwa na athari halisi, Umoja wa Ulaya unapaswa kulenga moja kwa moja Falme za Kiarabu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *