f

Chanzo cha picha, Getty Images

Rais wa Marekani Donald Trump ameondoa pendekezo lake la kutoza ada ya asilimia 20 kwa mizigo yote inayopitia Mlango wa Bahari wa Hormuz, akisema badala yake atategemea mikataba mikubwa ya biashara na uwekezaji kutoka mataifa ya Ghuba.

Hatua hiyo imekuja saa chache kabla ya Jeshi la Marekani kupitia Kamandi Kuu ya Marekani (CENTCOM) kurejesha kizuizi dhidi ya bandari za Iran na kuanzisha duru mpya ya mashambulizi dhidi ya malengo ya Iran.

CENTCOM ilisema mashambulizi hayo yanalenga kudhoofisha uwezo wa Iran wa kushambulia meli za kibiashara zinazopita katika Mlango wa Bahari wa Hormuz.

Mashambulizi hayo yanafuatia mapigano mapya kati ya Marekani na Iran, ambayo yamesababisha bei ya mafuta kupanda huku shughuli za usafirishaji wa mafuta kupitia Hormuz zikipungua kwa kiasi kikubwa.

Iran ilisema imelenga vituo vya kijeshi vya Marekani nchini Bahrain na Jordan, baada ya awali kushambulia meli mbili za Umoja wa Falme za Kiarabu.

Katika ujumbe aliouchapisha kwenye mtandao wa Truth Social, Trump alisema:

“Nimeamua kuondoa tozo ya asilimia 20 ya Marekani na badala yake mataifa ya Ghuba yatawekeza na kufanya mikataba mikubwa ya biashara nchini Marekani.”

Hata hivyo, hakutoa maelezo zaidi kuhusu mpango huo.

Trump pia alisema Mlango wa Bahari wa Hormuz utaendelea kuwa wazi kwa meli zote isipokuwa zile zinazofanya biashara na Iran.

Baadaye, akizungumza mjini Washington, Trump alisema hakupendelea wazo la kutoza ada kwa meli zinazopita Hormuz, lakini akaongeza kuwa si haki kwa Marekani kubeba jukumu la kulinda njia hiyo muhimu ya baharini kwa manufaa ya dunia nzima.

Kwa upande wake, Iran imesema itaendelea kusimamia Mlango wa Bahari wa Hormuz licha ya hatua za Marekani.

Unaweza kusoma;

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *