Kundi la wanajihadi la ADF linaendelea na ukatili wake mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC): mashambulizi kadhaa yalilenga eneo la Beni katika mkoa wa Kivu Kaskazini katika siku za hivi karibuni. Idadi ya vifo bado ni ya muda, lakini tayari kuna zaidi ya ishirini ambao inadaiwa wameuawa na kundi hili.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Na mwandishi wetu mjini Kinshasa, Paulina Zidi

Haya ni mashambulizi matatu tofauti yaliyolenga eneo la Beni mashariki mwa DRC. La kwanza lilitokea usiku wa Julai 12-13 na kulenga Beni, ambapo viongozi wa mkoa wa Kivu Kaskazini wamekuwa wakiishi tangu mji wa Goma kuanguka mikononi mwa kundi la waasi wa AFC/M23.

Watu wanaoshukiwa kuwa ADF—wapiganaji wa kijihadi wanaohusishwa na kundi la Islamic State—walifanya shambulio katika vitongoji vya Sayo na Matembo vya wilaya ya Mulekera, magharibi mwa jiji. Raia saba waliuawa, na wanajeshi watatu wa Jeshi la Kongo (FARDC) waliuawa katika shambulio la kuvizia.

Kisha, usiku wa Julai 14-15, mji wa Mangina ulilengwa. Ukiwa kaskazini zaidi katika eneo hilo, karibu kwenye mpaka kati ya mkoa wa Kivu Kaskazini na mkoa wa Ituri, wilaya hii ya vijijini iko kama kilomita 30 kutoka Beni. Wakati huu, kulingana na shirika la kiraia, raia wanne waliuawa.

Hatimaye, shambulio lingine lililenga mji wa Mangina siku ya Alhamisi. Idadi ya watu waliouawa ni kubwa: angalau raia 10 waliuawa kwa visu na mapanga- na hata kufikia kumi na moja, kiongozi wa shirika la kiraia aliiambia RF.

Watu waelekea katikati mwa jiji la Beni

Idadi ambayo bado ni ya muda: wafanyakazi wa uokoaji wanaendelea kutafuta maeneo yaliyoathiriwa. Na vurugu hizi mpya zimesababisha  watu kuelekea katikati mwa jiji la Beni, ambalo hadi sasa halijaathiriwa na mashambulizi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *