
Rais wa Marekani Donald Trump amelaani “udhaifu wa kushangaza” katika mfumo wa uchaguzi wa Marekani siku ya Alhamisi, Julai 16, akiinyooshea kidole China haswa. Miezi mitatu kabla ya uchaguzi wa katikati ya muhula mwezi Novemba, rais alizungumza, akidokeza mapema nia yake ya kupinga matokeo ya kura hii muhimu. Alitangaza kufutwa kwa hati, ingawa idara ya ujasusi ya Marekani haijapata ushahidi wowote wa China kuingilia uchaguzi huo.
Imechapishwa:
Dakika 2 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
“Hatuwezi tena kushuhudia uchaguzi mwingine uliogubikwa na udanganyifu,” rais alitangaza wakati wa hotuba yake, ambayo ilidumu kwa zaidi ya dakika 25, akidai kwamba mfumo wa uchaguzi umebaki kuwa kikwazo kikubwa kwa ukubwa wa Marekani. Kisha akarudia madai yake ambayo hayajathibitishwa kwamba uchaguzi wa urais wa 2020 uliibiwa kwa udanganyifu mkubwa kwa kumpitisha Joe Biden.
Aliilaumu China kwa kuingilia uchaguzi, ambayo alidai imekuwa ikiendelea kwa miaka kadhaa: “Kuanzia na uchaguzi wa mwaka 2020, China ilifanya kile kinachoonekana kuwa operesheni kubwa zaidi ya udukuzi wa data ya uchaguzi katika historia, na kusababisha China kupata faili milioni 220 za wapiga kura wa Marekani kinyume cha sheria,” aliongeza.
Kisha Donald Trump alidai kuwa na ushahidi wa kutosha wa kuingiliwa uchguzi kunakodaiwa kufichwa na “serikali kivuli”: nadharia ya njama ya hali ya juu inayofanya kazi dhidi yake.
Ujasusi haukupata ushahidi wa kuingiliwa kwa uchaguzi
Uchunguzi usiojulikana na huduma za ujasusi za Marekani kuanzia 2021 haukuonyesha ushahidi wowote unaoonyesha kwamba mhusika wa kigeni alijaribu au alifanikiwa kubadilisha “kipengele chochote cha kiufundi” cha uchaguzi wa rais wa 2020, iwe ni usajili wa wapiga kura, uchguzi, kuhesabu kura, au matokeo. Tathmini hii ilifanywa chini ya uongozi wa John Ratcliffe, wakati huo Mkurugenzi wa Ujasusi wa chini ya utawala wa Trump na sasa Mkurugenzi wa CIA.
Rais pia alishambulia mfumo wa uchaguzi, akilenga mashine za kielektroniki za kupiga kura na kuhesabu kura: “Ziko hatarini, ni rahisi kuziharibu, na watu katika serikali yetu walijua hilo.”
Tuhuma hizi si mapya, wala zile zinazodai kwamba wasio Wamarekani au hata watu waliotangazwa kuwa wamekufa walipiga kura. Kesi kama hizo zipo, lakini kwa kiwango kidogo sana kuliko kile kinachodaiwa na Donald Trump na bila kuathiri matokeo.
Bilionea huyo, ambaye hajawahi kukubali kushindwa kwake na Joe Biden mnamo mwaka 2020, aliwashutumu Wademocrats katika miezi ya hivi karibuni kwa kujaribu kuiba uchaguzi wa katikati ya muhula wa mwezi Novemba, ambapo Warepublican wanaweza kupoteza wingi wao mdogo katika Bunge.