BILA AMANI NA USALAMA HAKUNA MAENDELEO – RAIS SAMIA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema amani na usalama ni msingi mkuu wa maendeleo ya Taifa, akiwataka wananchi kuendelea kulinda tunu hizo ili kuhakikisha nchi inaendelea kuwa na mazingira bora ya ukuaji wa uchumi na ustawi wa jamii.

Rais Samia amesema hayo leo Jumatatu Julai 20, 2026 mkoani Kigoma wakati akizungumza mara baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Tabora hadi Kigoma na uzinduzi wa meli nne za mizigo katika Bandari ya Kigoma.

Amesema Serikali itaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo miundombinu ya usafiri na usafirishaji, lakini mafanikio ya miradi hiyo yanategemea uwepo wa amani na usalama nchini.

(Feed generated with FetchRSS)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *