Baada ya miaka minane ya uongozi wa shirika hilo, Audrey Azoulay anajiandaa kuachia ngazi. Halmashauri Kuu itamchagua mrithi wake leo Jumatatu, Oktoba 6. Wagombea wawili wako katika kinyang’anyiro: Mmisri Khaled El-Enany, anayeungwa mkono na mataifa makubwa kadhaa, na Firmin Matoko, raia wa Kongo, mwenye anayehudumu kwa miaka thelathini katika UNESCO. 

Imechapishwa:

Dakika 3 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Mbali na ushindani huu, changamoto ni nyingi kwa taasisi hii ambayo ni dhaifu, na ambayo inakabiliwa na ukosoaji mkubwa ambayo, kulingana na wataalam, inapaswa kujipanga upya kuhusu majukumu yake.

“Bii. Azoulay alipowasili mwaka wa 2017, alitekeleza mageuzi ya kimkakati, mabadiliko ya shirika ili kufanya UNESCO kuwa na ufanisi zaidi,” anakumbusha Oumar Keïta, balozi wa zamani wa Mali katika shirika hilo.

Katika kipindi cha miaka minane, Mfaransa Audrey Azoulay alifanya mageuzi mkubwa katika Shirika hili la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni (UNESCO). Bajeti yake imeongezeka maradufu, kutoka dola milioni 450 hadi milioni 900 kwa mwaka. Ameongeza mwonekano wa shirika la Umoja wa Mataifa na kuzindua miradi mikuu, kama vile ujenzi wa Mosul nchini Iraq. Pia alijikita katika urithi wa Kiafrika: maeneo 19 yameandikwa kwenye Orodha ya Urithi wa Dunia tangu mwaka 2018, ikilinganishwa na 11 tu chini ya mtangulizi wake. Maeneo thelathini na saba ya urithi wa Kiafrika yasiyoonekana pia yameongezwa kwenye orodha ya UNESCO, karibu nusu ya maeneo mapya yaliyoorodheshwa duniani kote.

Kwa wajumbe wa Uhispania, ulio karibu na Audrey Azoulay, shirika hilo, lililovuliwa misimamo yake ya kisiasa, “lina nguvu kuliko ilivyokuwa miaka minane iliyopita.” Lakini kuridhika huku hakufuti ukosoaji. Mtindo wa utawala wa Mkurugenzi Mkuu, unaochukuliwa kuwa “mgumu” na baadhi ya maafisa wa UNESCO, wakati mwingine umeonekana kuwa juu sana, na kuacha nafasi ndogo kwa mashirika yasiyo ya kiserikali na wajumbe wa nchi wanachama. “Amependelea hatua badala ya kushauriana,” amesema mwanadiplomasia mmoja, akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina.

Watafiti wana mtazamo kama huo. Mwanaanthropolojia Lynn Meskell anabaini kwamba UNESCO imekuwa “mateka kwa nchi wanachama wake,” lililogeuzwa na kuwa la shirika la kiufundi ambalo sasalinaepuka masuala nyeti. Katika kitabu chake, A Future in Ruins, anazungumzia “usimamizi wa mgogoro” na anatoa mfano wa Gaza: “Katika Gaza, karibu hakuna chochote, ni kidogo sana. UNESCO iliwahi kuwa na ujasiri wa kuchukua masuala haya, kutafuta mbinu za kuleta mataifa katika mazungumzo, kutafuta ufumbuzi, kuwajibika kwa kila mmoja. Leo, hakuna chochote kinachofanyika.” 

UNESCO, hata hivyo, inaangazia mipango kadhaa inayoendelea: ufuatiliaji wa uharibifu wa urithi wa kitamaduni, usaidizi wa kisaikolojia kwa wanafunzi, na usaidizi kwa wataalamu wa kitamaduni katika kulinda maeneo ya kiakiolojia. Kwa sababu ya ukosefu wa ufikiaji wa eneo hilo, hatua yake inabaki kuwa ndogo.

Kuhusu Mosul, mpango wa kujenga upya umesifiwa, lakini pia unashutumiwa kwa kukosa mizizi ya ndani: kulingana na uchunguzi wa mwaka 2018 uliofanywa na Lynn Meskell na msomi Benjamin Isakhan, 39% ya wakaazi waliona kuwa UNESCO haikuzingatia maoni yao vya kutosha.

Wagombea wawili, maono mawili

Ni kwa msingi huu ambapo wagombea wawili katika kinyang’anyiro hicho wanatafuta kujitofautisha, wakisisitiza sera ya “mlango ulio wazi”. Kulikuwa na wanne mwanzoni, lakini sasa wamebaki wawili tu. Kwa upande mmoja, Khaled El-Enany, 54, mtaalam wa Misri na waziri wa zamani, akiungwa mkono na Umoja wa Afrika, Jumuiya ya Kiarabu, na mataifa makubwa kadhaa, ikiwa ni pamoja na Ufaransa na Ujerumani. Kwa upande mwingine, Firmin Edouard Matoko, 69, afisa mkuu wa Kongo anayedai kufanya kazi kwa miaka thelathini katika UNESCO barani Afrika, Amerika Kusini, na Paris.

Wote wawili wanajionyesha kama wagombea wa mabadiliko. Khaled El-Enany anatetea “nyumba kwa watu wote” na anaahidi kusisitiza elimu, sayansi na mazungumzo. Mwanadiplomasia wa Uhispania, ambaye nchi yake inamuunga mkono mgombea huyo wa Misri, pia anasema ana imani naye kunyoosha fedha za shirika hilo.

Firmin Matoko, kwa upande wake, anategemea uzoefu na ujuzi wake wa ndani wa taasisi hiyo. “Mtu yeyote ambaye ameshughulikia nchi chache ana mwanzo,” anabainisha Oumar Keïta. Ahadi yake: “kufanya mageuzi bila kuhatarisha usalama,” kwa kuzingatia hasa maendeleo ya binadamu, vijana na wanawake.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *