
Bodi ya Utendaji ya UNESCO, siku ya Jumatatu, Oktoba 6, imemteua Mmisri Khaled el-Enany kuwa Mkurugenzi Mkuu wake kwa miaka minne ijayo, Mwenyekiti wa bodi hiyo, Vera El Khoury Lacoeuilhe, ametangaza. Mgombea huyo wa Misri alipata kura 55 dhidi ya 2 za Firmin Edouard Matoko kutoka Kongo, ameeleza.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Ilikuwa kura ya siri, kwa hiyo hatuwezi kujua kwa uhakika ni nchi gani ilimpigia kura mgombea yupi, lakini ushindi wa Khaled el-Enany ulikuwa wa wazi: kura 55 dhidi ya 2. Ni lazima isemwe kwamba yeye ndiye anayependwa zaidi, alikuwa akifanya kampeni za muda wote kwa miaka miwili, na alikuwa amepata uungwaji mkono wa umma kutoka kwa Muungano wa Nchi za Kiarabu, Umoja wa Afrika (AU), na nchi kama vile Brazil, Ufaransa, Ujerumani na Uturuki.
Kwa hivyo nivema kusema tu kwamba ahadi hizi za kupiga kura zilitekelezwa. Mgombea aliyeshindwa, Mkongo Firmin Édouard Matoko, aliingia kwenye kampeni akiwa amechelewa, miezi sita kabla ya kura, na kwa hivyo hakuweza kumpita mgombea aliyeshinda.
Mara tu baada ya kutoka kwenye ukumbi wa kikao, alitangaza kwa vyombo vya habari kwamba katika siku 100 za kwanza, atakutana na wawakilishi wote wa Nchi Wanachama ili kuandaa mpango mkakati. Kwanza, kushughulikia upunguzaji wa bajeti unaokadiriwa kuwa kati ya 8% na 11% kwa UNESCO kutokana na kujiondoa kwa Marekani mnamo mwaka 2026. Pili, kuboresha ufanisi wa taasisi hiyo, ambayo mara nyingi huchukuliwa kuwa ya urasimu. Mkurugenzi Mkuu mpya alitoa mawazo kadhaa, kama vile kuongeza vyanzo vya fedha kwa kuongeza ushiriki wa sekta binafsi kwa njia mbalimbali, na kisha kupitia ushirikiano zaidi kati ya mashirika.
Mkurugenzi Mkuu mpya ataanza kazi Novemba 14, akimrithi Audrey Azoulay. Ataidhishwa na Mkutano Mkuu wa UNESCO huko Samarkand, Uzbekistan, mnamo Novemba 9.