s

Chanzo cha picha, gp

    • Author, Na Mwandishi Wetu
    • Nafasi,

Rafiki yangu mmoja aliwahi kuishi jijini Doha, Qatar kwa takribani wiki moja. Aliporejea Dar es Salaam, nilimuuliza aniambie kwa nini aliamua kutofanya kazi aliyokuwa ameitiwa.

Jibu lake sijalisahau hadi leo; “Kazi ni nzuri na watu ni wazuri. Tatizo the place has no soul”. Kwa maelezo yake, mahali pale alipaona pa baridi, palipokosa uhai na uchangamfu wa Dar es Salaam.

Huwa nakumbuka hali hii kila nikikitazama Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) na ushiriki wake kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu ambapo tayari kimeteua mgombea urais na mgombea mwenza kwa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Wagombea wa CHAUMMA, Salum Mwalimu kwa urais na mgombea mwenza wake, Devotha Minja, ni waandishi wa habari maarufu wa Tanzania. Hii ndiyo mara ya kwanza katika historia ya Tanzania kwa wana habari wawili kupata fursa hii katika chama kimoja.



Source link

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *