Akieleza kuhusu makubaliano ya kusitishwa mapigano, Erdogan alisisitiza kuwa “kilicho muhimu kwa sasa ni kuhakikisha kuwa makubaliano hayo yanatekelezwa kikamilifu,” akiongeza kuwa Uturuki itachangia pakubwa katika mchakato huo.

“Kanda yetu, na hasa Gaza, imestahmili umwagikaji damu wa kutosha, mauaji ya kikatili, na majonzi,” amesema. “Amani lazima ipewe nafasi, hatua zozote za kukiuka makubaliano ziepukwe.”

Erdogan alieleza makubaliano hayo kama “hatua kubwa” katika kufikia amani ya kudumu licha ya changamoto zilizopo mbele. “Mlango wa kupatikana kwa amani ya kudumu Gaza umefunguliwa,” alisema. “Tunasema — hakuna tena umwagikaji damu.

Marekani imethibitisha kuwa jeshi la Israel limekamilisha awamu ya kwanza ya kuondoka hadi kwenye mstari wa njano. Chini ya makubaliano hayo, Hamas inatakiwa kuwaachiliwa huru mateka 20 na kurejesha miili 28, huku Israel ikiwaachilia huru wafungwa wa Palestina 250 waliohukumiwa vifungo vya maisha na 1,700 waliokamatwa tangu Oktoba 7, 2023.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *