
Mchezaji huyu kiungo mkabaji anajulikana kama ‘‘Dokta’’ kutokana na utaalamu wake uwanjani.
‘‘Dokta’’ Aucho amewahi kucheza katika timu nyingi ikiwemo Water FC ya Uganda, Simba ya Uganda, Tusker FC na Gor Mahia za Kenya na Baroka ya Afrika Kusini.
Kama ulikuwa hufahamu Khalid Aucho amecheza katika Ligi zingine ambazo pengine hujawahi kuzisikia. Fundi huyu mwenye umri wa miaka 32 amecheza katika ligi ya Serbia na timu ya ligi daraja la pili ya Misri ya Misr lel-Makkasa.
Pengine mmezoea India kuna sinema za Bollywood au kriketi, Dokta Aucho alicheza pia huko akiwa na timu za East Bengal na Churchill Brothers.
Lakini ni wazi nyota yake iling’aa zaidi alipojiunga na Wananchi, mabingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania, Young Africans mwaka 2021.