
Akizungumza akiwa kwenye makaazi yake ya mapumziko nje kidogo ya mji wa Roma, Baba Mtakatifu Leo amesema anarejea ombi lake kwa watu wote wenye nia njema kuifanya Krismasi kuwa siku ya amani, kwa angalau kuonesha heshima kwa siku hiyo ya kuzaliwa Yesu Kristo.
Papa Leo pia ameelezea masikikito yake makubwa kwamba Urusi imekataa kuweka chini silaha kwenye vita vinavyoendelea nchini Ukraine hata wakati wa Krismasi.
Wakristo duniani watasherehekea sikukuu ya Krismasi hapo kesho kukumbuka kuzaliwa kwa Yesu zaidi miaka 2000 iliyopita.