Kwa kipindi cha miaka 30, Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasi­si za Fedha, Huduma na Ushauri (TUICO) kimejijengea historia ya kipekee kama nguzo muhimu ya ulinzi wa haki, maslahi na utu wa wafanyakazi nchini.

Tangu kuanzishwa kwake, TUICO imekuwa mstari wa mbele katika kusimamia haki za wafanyakazi, kushawishi sera bora za ajira na kujenga mahusiano imara kati ya wafanyakazi, waajiri na Serikali.

TUICO ni chama huru kilichosa­jiliwa chini na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Wafanyakazi Tanzania, kwa lengo la kudai, kulinda na kute­tea haki, heshima na maslahi ya wanachama wake na wafanyakazi kwa ujumla. TUICO kiliundwa ras­mi mwaka 1995 kufuatia Mkutano Mkuu uliofanyika jijini Arusha. Mpaka kufikia mwaka 2025 chama kimetimiza miaka 30 ya uhai wake.

TUICO kilianzishwa katika mazin­gira ambayo wafanyakazi waliku­wa wakikabiliwa na changamoto nyingi, ikiwemo ukosefu wa ulinzi wa kutosha wa kisheria, mazingira duni ya kazi na sauti dhaifu katika maamuzi yanayohusu ajira. Kuan­zishwa kwa TUICO kulilenga kuun­ganisha sauti za wafanyakazi chini ya mwavuli mmoja wenye nguvu, ili kuhakikisha haki zao zinalindwa na kusikilizwa.

Kwa miaka ya awali, TUICO ilijik­ita zaidi katika kujenga mifumo ya uendeshaji, kuimarisha uanachama na kutoa elimu ya haki za kazi kwa wafanyakazi katika sekta mbalim­bali, ikiwemo viwanda, biashara, huduma na taasisi za fedha.

Katika miaka 30 chama kime­pata mafanikio makubwa ambayo kwa muda huu mfupi ni vigumu kuyaorodhesha yote. Hata hivyo kwa kifupi ni kama ifuatavyo:-

Chama kimehamasisha wafanya­kazi kujiunga na Chama na sasa kina wanachama 150,000 ambao ni mafanikio makubwa kwani kili­poanza kilikuwa na wanachama 30,000 ambao kiliwarithi kutoka OTTU.

Chama sasa kinahudumia wana­chama katika Sekta nne ambazo ni Sekta ya Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha na Huduma na Ushauri wakati kilikuwa na sekta mbili tu yaani Sekta ya Viwanda na Biashara wakati kinaanza.

Chama kina ofisi katika mikoa mikubwa 22, ofisi ndogo tano na ofisi ya Makao Makuu. Ofisi zote zina watumishi wa kutosha wenye weledi na vitendea kazi ikiwemo usafiri wa uhakika hivyo huduma kuwafikia wanachama katika ubora mkubwa na unaokubalika.

Chama kinaongoza kwa kufun­ga mikataba ya hali bora za kazi. Chama kimefikia uwezo wa kufunga mikataba kati ya 80 – 100 kwa mwa­ka. Mikataba hii huboresha maslali ya wafanyakazi mahala pa kazi.

TUICO kimekuwa mstari wa mbele kutatua migogoro ya wafa­nyakazi mahali pa kazi katika ngazi mbalimbali za kutoa haki. Chama kimekuwa kikipokea migogoro takribani 320 kwa mwaka. Kupitia chama wafanyakazi wengi hupata haki na maslahi yao.

Chama kimekuwa kikitoa mafun­zo kwa wafanyakazi, wanachama na waajiri juu ya masuala ya vyama vya wafanyakazi. Kwa sasa Chama huendesha semina zaidi ya 10,000 kwa mwaka. Semina hizi huwajen­gea uwezo washiriki na kupunguza migogoro mahali pa kazi.

Chama kimeendelea kujenga uhu­siano mwema na Serikali inayoon­gozwa na Dk Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wadau mbalimbali wa ndani na nje ya nchi kama TUC­TA, ATE, ILO, FES, IndustriAll, PSI, DTDA, FNV, BWI, IUF na mashi­kikisho mengine Duniani. Chama kimepata uzoefu mkubwa katika uendeshaji wa shughuliu za Vyama vya Wafanyakazi.

Chama kinashiriki kikamilifu tan­gu kuanzishwa kwake katika taasisi za utatu kama vile Tume ya Usuluhi­shi na Uamuzi (CMA) Bodi za Kima cha Chini cha Mshahara (Wage Boards) Baraza la Kazi, Uchumi na Jamii (LESCO), Kamati ya Huduma Muhimu (Essential Services Com­mittee) na bodi mbalimbali katika taasisi za Umma, hivyo kuimarisha utatu wetu.

Safari ya miaka 30 haijakosa changamoto. TUICO imekumba­na na mabadiliko ya kiuchumi, mageuzi ya sera, ushindani wa soko huria na wakati mwingine mazin­gira magumu ya ajira. Hata hivyo, changamoto hizo zimekuwa chachu ya mageuzi, ubunifu na uimara wa shirikisho.

Katika kuadhimisha miaka 30, TUICO inaingia hatua mpya yenye dira ya kuimarisha zaidi ulinzi wa wafanyakazi katika ulimwengu unaobadilika kwa kasi, hasa kati­ka nyanja za teknolojia, ajira zisizo rasmi na uchumi wa kidijitali.

Dhamira ya TUICO inaendelea kuwa ileile: kutetea haki, utu na ust­awi wa wanachama wake na wafa­nyakazi kwa ujumla nchini, huku ikijenga ushirikiano imara kwa maendeleo endelevu ya taifa.

Safari ya miaka 30 ya TUICO ni ushuhuda wa nguvu ya mshika­mano wa wafanyakazi. Ni histo­ria ya mapambano, mafanikio na matumaini mapya. Kadri chama kinavyoendelea kusonga mbele, kinaendelea kubaki kuwa sauti ya wafanyakazi na nguzo muhimu ya haki na maendeleo ya kijamii nchini Tanzania.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *