Timu ya wanasayansi wa kimataifa imesema Ijumaa kwamba bahari za dunia zilifyonza kiwango kikubwa cha joto mwaka 2025 na hivyo kuchochea hali ya kuongezeka kwa kina cha bahari, dhoruba kali na matumbawe kufa.

Joto ambalo limekusanyika baharini mwaka jana liliongezeka kwa takriban zettajouli 23 — kiasi sawa na karibu cha miongo minne ya matumizi ya nishati msingi duniani.

Ugunduzi huu — uliochapishwa katika jarida la Advances in Atmospheric Sciences — ulionyesha kiwango cha juu zaidi ya mwaka wowote tangu kulipoanzishwa utunzaji wa kumbukumbu za kisasa mapema miaka ya 1950, watafiti walisema.

Ubelgiji | Visiwa vya Scheldt huko Antwerp
Vivuko vya Scheldt huko Antwerp vinarejeshwa kama sehemu ya Mpango wa kulinda jiji kutokana na kuongezeka kwa vina vya bahari na mabadiliko ya mawimbi katika lango la Scheldt.Picha: Thomas Bruyninck

Zaidi ya wanasayansi 50 kutoka taasisi 31 za utafiti walitumia vyanzo vingi ikiwa ni pamoja na roboti elfu moja zinazoelea zikifuatilia mabadiliko ya bahari hadi kina cha mita 2,000.

Karina von Schuckmann, mwandishi mwenza wa utafiti huo alisema kuchunguza kina, badala ya mabadiliko ya uso wa bahari, hutoa kiashiria bora zaidi cha jinsi bahari zinavyokabiliana na “shinikizo endelevu” kutokana na uzalishaji wa hewa chafu kutoka kwa binadamu

“Taswira iko wazi: matokeo ya 2025 yanathibitisha kwamba bahari inaendelea kupata joto,” von Schuckmann, mtaalamu wa bahari kutoka taasisi ya utafiti ya Ufaransa Mercator Ocean International, aliiambia AFP.

Italia Milani 2025 | Watalii wakijipoza kwenye chemchemi ya kihistoria ya maji kufuatia wimbi la joto
Watalii wakijipoza na maji kutokana na joto kali katika mji wa Milan, ItaliaPicha: Francesco Enriquez/Independent Photo Agency Int./IMAGO

Bahari ndio mdhibiti mkuu wa joto duniani

Bahari ni mdhibiti mkuu wa hali ya hewa ya Dunia kwa sababu hunyonya asilimia 90 ya joto la ziada katika anga linalosababishwa na usambazwaji wa gesi chafu kama vile kaboni.

Nishati hiyo yote ya ziada ina athari kubwa. Bahari zenye joto huongeza unyevunyevu angani, na kutoa nishati inayochochea vimbunga vya kitropiki na mvua zinazoleta madhara makubwa.

Bahari zenye joto zaidi pia huchangia moja kwa moja katika kuongezeka kwa kina cha bahari — maji huongezeka yanapopata joto — na kufanya hali kuwa ngumu kwenye miamba ya kitropiki, ambayo matumbawe yake huangamia kunapotokea mawimbi ya joto ya baharini kwa muda mrefu.

Marekani Honolulu 2025 | Mawimbi katika Ufuo wa Waikiki baada ya tahadhari ya tsunami
Mawimbi yakigonga ukuta wa bahari karibu na Ufuo wa Waikiki baada ya mamlaka kupunguza kiwango cha tahadhari ya awali ya tsunami kufuatia tetemeko la ardhi karibu na Rasi ya Kamchatka Mashariki mwa Urusi, huko Honolulu, Hawaii, Marekani, Julai 30, 2025.Picha: Marco Garcia/REUTERS

“Ikiwa Dunia itaendelea kuongeza joto, kiwango cha joto baharini pia kitaendelea kuongezeka, kina cha bahari kitaongezeka na kutakuwepo na rekodi mpya,” alisema von Schuckmann.

Chaguo la binadamu

Ongezeko la joto baharini linatofautiana, kwa kuwa baadhi ya maeneo hupata joto haraka zaidi kuliko mengine. Bahari za kitropiki, Atlantiki Kusini, Mediterania, Bahari ya Hindi kaskazini na Bahari ya Kusini zilikuwa miongoni mwa maji yaliyochukua kiwango cha juu zaidi cha joto kilichorekodiwa mwaka wa 2025.

Mradi tu ongezeko la joto duniani halitashughulikiwa na kiasi cha joto kilichonaswa angani kitaendelea kuongezeka, bahari vina vya bahari vitaendelea kuongezeka kwa viwango visivyovumilika, watafiti walisema.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *