
Balozi wa Uturuki nchini Syria Nuh Yilmaz alisema siku ya Ijumaa kuwa inaridhisha kuona kuwa makubaliano ya Aprili 1 hatimae yanatekelezwa Aleppo, Syria.
“Inaridhisha kuona kuwa makubaliano ya Aprili 1, ambayo yanalenga kupatikana kwa amani na utulivu Aleppo, hatimae yanatekelezwa, ingawa kwa kuchelewa na kwa uzito,” Yilmaz alisema katika ujumbe kupitia mtandao wa kijamii wa Marekani X.
Akieleza kuhusu makubaliano yaliyofikiwa mwaka uliopita kati ya serikali ya Syria na kundi la kigaidi la YPG/SDF kuhusu kundi hilo kuondoka maeneo ya Sheikh Maksoud na Ashrafiyeh Aleppo, Yilmaz alisema: “Usalama, umoja na utulivu utatupeleka katika kupatikana kwa mustakbali bora.”
Kundi la kigaidi la YPG/SDF limekuwa likishambulia maeneo kadhaa Aleppo kutoka maeneo ambayo wanayadhibiti tangu Disemba 6.