Ethiopia itazindua Bwawa lake la Grand Renaissance leo Jumanne, Septemba 9. Jiwe la msingi liliwekwa mwaka wa 2011. Bwawa hilo ambalo linapatikana kaskazini mashariki mwa nchi, madhumuni yake rasmi ni kuzalisha umeme kwa ajili ya Ethiopia, ambapo karibu nusu ya wakazi hawana umeme. Lakini zaidi ya yote, inakusudiwa kuwezesha nchi kujiimarisha kama msambazaji wa umeme wa kikanda.

Imechapishwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Nchini Ethiopia, huu ni utekelezaji wa mradi mkubwa. Bwawa hili lenye Urefu wa kilomita 1.8, urefu wa juu wa mita 145, na linajumuisha mitambo 16, na kufanya uwezo wa uzalishaji kufikia megawati 5,000, sawa na zaidi ya vinu vya nyuklia vitatu. Bwawa hili linatajwa kuwa ndilo lenye nguvu zaidi barani Afrika. Kukamilika kwake, kulitangazwa Julai 3 na Abiy Ahmed mbele ya Bunge, kunaashiria mwisho wa mradi wa ajabu ambao ulipangwa kukamilika mnamo mwaka 2017.

Kwa gharama ya karibu dola bilioni tano, mradi huu umekumbwa na ucheleweshaji mwingi, haswa kutokana na matatizo ya utekelezaji, lakini pia masuala ya kifedha, na mivutano ya kijiografia. Bwawa la Grand Renaissance linapatikana kwenye Nile ya Bluu, limesabbisha mvutano mkubwa na Misri, ambayo inategemea karibu kabisa na mto kwa mahitaji yake. Cairo inashikilia kuwa bwawa hilo linawakilisha tishio “lililopo”, kwani linategemea 97% ya mahitaji yake ya maji kwenye Mto Nile na inahofia inaweza kusababisha kukauka kwa chanzo chake kikuu cha usambazaji.

Mfano wa mafanikio ya kitaifa, kulingana na mamlaka

Bwawa la Grand Renaissance linatarajiwa kuongeza maradufu uzalishaji wa sasa wa umeme nchini humo. Wakati inakusudiwa ŕasmi kuendeleza usambazaji wa umeme wa ndani—kaŕibu nusu ya wakazi wanaishi bila umeme, kulingana na Benki ya Dunia—kuna uwezekano, kulingana na wataalam, kwamba sehemu kubwa itauzwa nje ya nchi kikanda ili kuruhusu Addis Ababa kuingiza fedha za kigeni.

Bwawa hilo linakuzwa na mamlaka kama mfano wa mafanikio ya kitaifa. Katika mahojiano ya hivi majuzi ya televisheni, Abiy Ahmed alisema kwamba anatarajia bwawa hilo kuzalisha mapato ya dola bilioni 1 kila mwaka, kiasi ambacho wataalam wanabainisha kuwa kinakadiriwa kupita kiasi. Waziri Mkuu aliongeza kuwa miradi mingine ya aina hii inatarajiwa kuanzishwa katika miaka ijayo.

Mradi unaochochea mivutano ya kikanda

Kwa takriban miaka kumi na tano, Misri imefanya kila iwezalo kuzuia mradi huu. Nchi hiyo imedai haki za kihistoria zilizorithiwa kutoka enzi ya ukoloni iliyoanzia zaidi ya karne moja. Rais Abdel Fattah al-Sisi hatakuwepo kwenye sherehe hizo, wala mwenzake wa Sudan hatakuwepo. Nchi zote mbili ziko chini ya mto kutoka bwawa, na bwawa liko kilomita chache kutoka mpaka wa Sudan. Khartoum ilionyesa upinzani wake hivi majuzi, kutokana na hofu ya mafuriko na usumbufu wa mabwawa yake na matumaini ya nishati nafuu.

Ili kushinda vita vya kidiplomasia, Ethiopia imeweza kupata washirika kati ya nchi nyingine ambazo Mto Nile unapita na ziko juu ya mto huo, kama vile Uganda na Tanzania, ambazo changamoto ya mikataba ya kikoloni inatoa fursa.

Bwawa la Renaissance lilijengwa kwa rasilimali za kitaifa. Kwa sababu ya kutokubaliana na Misri, mashirika mengi ya kimataifa yalikataa kufadhili ujenzi huo. Kwa hivyo, kwa Waethiopia, inawakilisha ishara yenye nguvu ya uhuru na uhuru wa nchi.

“Utekelezaji wa mradi huu umezua mvutano mkubwa wa kikanda, na kuzua hofu nchini Sudan na Misri kuhusu athari zake katika mtiririko wa Blue Nile. Hata hivyo, hakuna shaka kwamba huu ni wakati muhimu sana kwa Waethiopia” , anasema Tsegay Tekleselassie, mwanauchumi katika Chuo cha Wellesley nchini Marekani.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *