Baraza la Katiba nchini Côte d’Ivoire limechapisha orodha ya mwisho ya wagombea katika uchaguzi wa urais wa Oktoba 25. Wagombea watano wameidhinishwa, Tidjane Thiam na Laurent Gbagbo wakikataliwa.

Imechapishwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Orodha ya mwisho ni pamoja na majina ya rais aliyeko madarakani na mgombea wa muhula wa nne, Alassane Ouattara; Simone Ehivet, mke wa zamani wa Laurent Gbagbo; Henriette Lagou, waziri wa zamani ambaye pia alikuwa mgombea mwaka 2015; Jean-Louis Billon, Waziri wa zamani wa Biashara, ambaye anaungwa mkono na Democratic Congress, muungano wa vyama vinane vya kisiasa; na Ahoua Don Mello, mwanaharakati wa PPA-CI, ambaye alikataliwa na chama chake, akijjichagulisha kama “mgombea wa tahadhari.” Hii inaangazia uwepo wa wanawake wawili katika uchaguzi huu wa urais.

Chantal Camara, Rais wa Baraza la Katiba, alishughulikia suala moja: kuruhusiwa kwa kila mgombea. Kwa jumla, kulikuwa na  faili 60. Faili kadhaa zilichukuliwa kuwa hazikubaliki kwa sababu ya kutokamilika. Baadhi ya wwagombea hawakutimiza umri wa chini wa miaka 35 na kwa hivyo walikataliwa.

Baraza la Katiba pia lilikataa kugombea kwa Tidjane Thiam na Laurent Gbagbo. Taasisi hiyo iliona faili zao kuwa zisizokubalika kwa sababu “ni lazima mtu awe mpiga kura mwenye ubora na aandikishwe ipasavyo kwenye orodha ya wapigakura,” alisema Chantal Camara, Rais wa taasisi hiyo. Hakika, Laurent Gbagbo aliondolewa kwenye orodha ya wapiga kura mwaka 2020, kufuatia kutiwa hatiani na mahakama za Côte d’Ivoire. Kinachoongezwa kwa hili ni “nakisi” ya baadhi ya ridhaa 20,000 katika faili yake. Tidjane Thiam, kwa upande wake, aliondolewa mwezi Juni 2025 kutokana na masuala ya utawala. Uamuzi wa mahakama ulisema kwamba hakuwa tena raia wa Côte d’Ivoire wakati wa kuandikishwa kwake. Baraza la Katiba lilikataa hoja zote zilizowasilishwa na pande hizi mbili.

Hakuna rufaa zaidi inayowezekana

Katika hatua hii, hakuna rufaa zaidi inayowezekana kwao. Hatimaye, vyama viwili vikuu vya upinzani, PDCI na PPA-CI, vinajikuta bila mgombea katika uchaguzi wa urais wa mwezi Oktoba. Hadi wakati huo walikuwa wameondoa chaguo la Mpango B. Watu ambao walikuwa wameelezea matarajio yao ndani ya vyama hivi waliidhinishwa: Jean-Louis Billon na Ahoua Don Mello, ambaye anagombea kama “mgombea wa tahadhari,” ili kuepuka chama chake, PPA-CI, “kisikose kwenye kinyang’anyiro hiki.” Baada ya muda mfupi tu, viongozi hawa wawili wa kisiasa walikataliwa na vyama vyao, ambavyo viliwafuta kwenye nafasi zao.

Mnamo mwaka 2020, faili kadhaa zilikataliwa kwa sababu ya mapungufu ya ufadhili. Baraza la Kikatiba lilikataa fomu za usajili wa wapigakura zilizokuwa na makosa katika kuwatambua wapigakura au nakala rudufu ya maingizo. Hii inaelezea kukataliwa kwa ugombea wa Waziri Mkuu wa zamani Pascal Affi N’Guessan. Baraza la Katiba lilibaini mapendekezo kadhaa batili. Kwa jumla, karibu uidhinishaji 20,000 haupo ili faili yake ichukuliwe kuwa inakubalika. Wagombea wengine wawili wa kujitegemea, Antoine Tiémoko Assalé na Vincent Toh Bi Irié, failiao zilikataliwa kwa sababu kama hizo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *