Kulingana na Mwiru, yeyote atakayefanya vitendo vya kifisadi, ataenda kukutana na mamba kwenye ikulu yake, akiahidi kumtumbukiza yeyote atakayejihusisha na ufisadi na uhujumu uchumi ndani ya bwawa hilo.

“Kama umewatesa Watanzania wenzako kwa muda mrefu, mtu anakula pesa za zahanati 5, zahanati 6, leo mnamwacha anatembea, eti anavinjari mtaani, atakutana na kitanzi cha Rais. Ni lazima nitamdumbukiza kwenye bwawa la mamba, apambane na mamba,” aliongeza.

Kwa mujibu wa Tume Huru ya Uchaguzi Tanzania (INEC), jumla ya vyama vya siasa 18 vitashiriki Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2025, huku vyama 17 vikisimamisha wagombea Urais.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *