Safari za ndege zimeanza tena Jumanne asubuhi kutoka viwanja vya ndege vya Copenhagen na Oslo baada ya sitofahamu siku ya Jumatatu jioni kutokana na ndege zisizo na rubani kuonekana juu ya anga ya Denmark. Serikali ya Denmark imeshutumu”shambulio kubwa zaidi kwenye miundombinu muhimu.”

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Baada ya Jumatatu jioni yenye matukio mengi mabaya na kusitishwa kwa safari za ndege katika viwanja vya ndege vya Copenhagen na Oslo kutokana na ndege zisizo na rubani juu ya anga ya Denmark, safari za ndege zimeanza tena leo Jumanne. Waziri Mkuu wa Denmark ameshutumu tukio hilo Jumanne kama “shambulio baya zaidi kwenye miundombinu muhimu” nchini Denmark. “Hii inalingana na mtindo ambao tumeona hivi majuzi na mashambulizi mengine ya ndege zisizo na rubani, ukiukaji wa anga, na mashambulizi ya mtandaoni dhidi ya viwanja vya ndege vya Ulaya,” amesema Mette Frederiksen, akirejelea matukio sawa na hayo nchini Poland na Romania na uvamizi wa Urusi wa ndege za kivita za Urusi katika anga ya Estonia.

Kwa upande wake, Norway imeishutumu Urusi kwa kuwa tayari imekiuka anga yake mara tatu mwaka huu. “Urusi imekiuka anga ya Norway mara tatu msimu huu wa joto na kiangazi,” Waziri Mkuu wa Norway Jonas Gahr Støre amesema katika taarifa. “Hatuwezi kuamua ikiwa hii ilikuwa kitendo cha makusudi au hitilafu ya urambazaji. Haijalishi sababu gani, hii bado haikubaliki, na tumeweka wazi hili kwa mamlaka ya Urusi,” ameongeza.

“Tunakabiliwa na tishio kubwa la hujuma nchini Denmark,” amesema Mkurugenzi wa operesheni katika idara ya Ujasusi ya Denmark (PET), Flemming Drejer, katika mkutano na waandishi wa habari. Kwenye mtandao wa kijamii wa X, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ameshutumu ukiukaji wa anga ya Denmark uliofanywa na Urusi. Hata hivyo inakanusha madai hayo na kusema kuwa haihusiki. “Kila wakati, tunasikia shutuma zisizo na msingi,” amesema msemaji wa Kremlin Dmitry Peskov.

Safari 100 za ndege zilifutwa

Tukio hilo lilisababisha usumbufu kwa abiria 20,000, kulingana na mamlaka. Safari za ndege thelathini na moja zilielekezwa kwenye viwanja vingine vya ndege na 100 kufutwa. 

Ndege hizi zisizo na rubani zilikuwa zikitoka pande tofauti, Bw. Jespersen ameongeza, akibainisha kwamba ziliweza kupaa kutoka kwenye meli iliyokuwa imeegeshwa baharini. Uwanja wa ndege wa Copenhagen uko kwenye pwani ya Mlango-Bahari wa Oresund, kati ya Sweden na Denmark. Ulifungwa siku ya Jumatatu jioni saa 2:30 usiku na kufunguliwa tena muda mfupi baada ya saa sita usiku. Hapo awali, polisi wa Copenhagen walisema walikuwa wakishirikiana na wenzao huko Oslo baada ya kuonekana kwa ndege zisizo na rubani katika mji mkuu wa Norway pia kusababisha uwanja wa ndege kufungwa kwa saa kadhaa. Idara za ujasusi za Norway zimethibitisha kuhusika kwao katika uchunguzi huo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *