Tangu Septemba 27, waandamanaji wamekuwepo barabarani katika miji kadhaa nchini Morocco, wakipinga matumizi ya mabilioni ya fedha yanayoelekezwa katika maandalizi ya Kombe la Dunia 2030.

Vijana hao wanaojiita wanaharakati wa “Gen Z 212” wamekuwa wakiandamana katika maeneo ya viwanja vipya wakidai kutelekezwa kwa huduma za msingi za umma. Vijana hao wamehamasishana kupitia mitandao ya kijamii kama TikTok na mingineyo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *