Msimu wa 2024-25 wa winga teleza Dembele uliimarika zaidi ikawa kama kurutubisha kipaji chake. Aliifungia timu yake magoli 33 na kusaidia kutoa pasi zilosababisha kupatikana kwa magoli 15 katika mechi 49 alizocheza PSG.

Alichaguliwa mchezaji bora wa mwaka wa Ligi Kuu ya Ufaransa Ligue 1 na mchezaji bora wa msimu wa Ligi ya Mabingwa barani Ulaya, pamoja na kumaliza msimu akiwa mfungaji bora.

Mafanikio haya yalimfanya ashinde tuzo ya juu katika soka ya Ballon d’Or mwaka 2025.

Masour Ousmane Dembele ni mzaliwa wa eneo la Vernon, Eure, kanda ya Normandy, Kaskazini mwa Ufaransa. Asili ya mama yake ni Mauritania na Senegal na baba yake mzazi ni wa asili ya kutoka nchi ya Mali.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *