#HABARI: Mwanafunzi wa chuo mkoani Tabora amefariki papo hapo katika ajali ya mwendesha pikipiki (bodaboda) aliyegonga Treni ya abiria iliyokuwa ikitoka Tabora kuelekea Mkoa wa Katavi.

Afisa Mnadhimu wa Jeshi la Zimamoto na uokoaji mkoani hapo Omary Simba wakati wakiendelea na harakati za kuokoa waathirikia wa ajali hiyo iliyotokea maeneo ya Isevya Manispaa ya Tabora kwenye makutano ya Reli na Barabara za vyombo vingine vya moto, amethibitisha kutokea kwa kifo hicho huku Dereva wa pikipiki akijeruhiwa na kuwahishwa hospitalini.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *