Mvutano wa kidiplomasia unaendelea kuchacha kati ya Uganda na Marekani, na chanzo chake kilianzia mitandaoni.

Kiini cha mgogoro huo ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba, ambaye alichapisha ujumbe kwenye mitandao ya kijamii akidai kuwa Ubalozi wa Marekani mjini Kampala umeingilia masuala ya ndani ya kisiasa ya Uganda.

Mkuu huyo wa jeshi, ambaye pia ni mwana wa Rais Yoweri Museveni, alipendekeza kusitishwa kwa ushirikiano wa kijeshi kati ya Kampala na Washington, ikiwemo operesheni zao za pamoja za kiusalama katika eneo la Pembe ya Afrika.

Machapisho hayo pia yalimhusu mwanasiasa wa upinzani Bobi Wine na mara moja yakazua mjadala na mabishano makali. Ndani ya saa chache, ujumbe huo ulifutwa.

“Taarifa zisizo sahihi”

Baadaye, Jenerali Muhoozi alisema kuwa taarifa alizotegemea hazikuwa sahihi, na akathibitisha kuwa ushirikiano wa kijeshi kati ya Uganda na Marekani “utaendelea kama kawaida”.

Hata hivyo, huko Washington, maelezo hayo hayakutosha kutuliza wasiwasi. Mwenyekiti wa Kamati ya Mahusiano ya Kigeni ya Seneti ya Marekani, Seneta Jim Risch, alisema kuwa Jenerali Kainerugaba “amevuka mstari mwekundu”.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *