Msitu wa Karura ambao unapatikana katikati ya mji mkuu, Nairobi, hekta zake 1,000 zinawakilisha msitu wa pili kwa ukubwa wa mijini duniani. Karura ilianzishwa miaka ya 1990 baada ya mapambano marefu yaliyoongozwa na jamii za wenyeji na mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel Wangari Mathai. Wiki hii, serikali ilitangaza kuwa imesafisha zaidi ya hekta moja ya hifadhi hii ili kuweka kitalu cha miti na nyumba za malazi kwa ajili ya Huduma ya taifa ya Vijana.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Na mwandishi wetu jijini Nairobi, Gaëlle Laleix

Friends of Karura ni chama cha jamii za wenyeji ambacho kimesimamia msitu huo, kwa ushirikiano na serikali ya Kenya, tangu miaka ya 2000. Hata hivyo, mlio wa tingatinga ndio uliwatahadharisha wanachama wake kuhusu kukatwa kwa sehemu ya msitu huo. “Tunashangaa kwa nini,” anasema Profesa Karanja Njoroge, kiongozi wa zamani wa chama hicho.

Kulingana na serikali, eneo hili litatumika kuunda kitalu cha miti, kinachokusudiwa kutoa miche milioni kadhaa kwa mwaka. Hili ni jambo la lazima ili kufikia lengo la serikali la kupanda miti bilioni 15 ifikapo mwaka wa 2032, kulingana na Wizara ya Mazingira.

Shirika lisilo la kiserikali la Green Belt Movement limeelezea kwenye mtandao wa kijamii wa X, kejeli ya kusafisha msitu uliokomaa kwa kutumia kivuli cha kupanda tena miti kwingineko. Pia lina wasiwasi kuhusu mradi huu wa kujenga nyumba za malazi kwa ajili ya Huduma ya taifa ya Vijana na linashangaa kusikia kwamba ni marufuku kurekodi au kupiga picha za eneo la ujenzi.

Mnamo mwezi Septemba, serikali ya Kenya ilijaribu kuwaondoa Marafiki wa Karura kutoka kwa usimamizi wao wa pamoja wa msitu huo. Wiki chache mapema, mahakama ya Kenya ilizuia mradi wa upanuzi wa barabara ambao katika hifadhi hii ya ikolojia.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *