Chanzo cha picha, EPA
Mkuu wa
jeshi la Iran Amir Hatami ametishia kuanza kulipiza kisasi “madhubuti” kwa mauaji ya mkuu wa usalama Ali Larijani katika
shambulio la anga la Israel.
“Kwa
wakati na mahali mwafaka, jibu la uamuzi, la kuzuia, na la kujutia litatolewa
kwa Marekani ya jinai na utawala wa Kizayuni wenye kiu ya umwagaji damu,”
Hatami alisema katika taarifa yake.
Aliongeza
kuwa Larijani na vifo vya “mashahidi wengine vitalipizwa kisasi”.
Walinzi
wa Mapinduzi wa Iran, ambao ni tofauti na jeshi, wanasema tayari wamerusha
makombora katikati mwa Israeli “kulipiza kisasi” kwa kifo cha
Larijani, shirika la habari la AFP linaripoti.