Maandamano makubwa yamepangwa kufanyika alasiri ya Jumamosi, Machi 21, huko Prague dhidi ya serikali ya bilionea Andrej Babis. Waandaaji, wakitarajia kukusanya hadi watu 400,000, wanaushutumu muungano wake kwa kushambulia baadhi ya misingi ya demokrasia na utawala wa sheria. Hivi majuzi, sheria iliyopendekezwa kuhusu hadhi ya mashirika yasiyo ya kiserikali imezua hofu na ukosoaji.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Na mwandishi wetu huko Prague, Alexis Rosenzweig

Vitisho kwa shirika la utangazaji wa umma, shinikizo kwa Rais wa Jamhuri, na sasa rasimu ya sheria inayolenga kudhibiti vikali shughuli za mashirika yasiyo ya kiserikali, ikiwataka kujiandikisha katika sajili maalum kwa ufadhili wowote au hata mawasiliano na vyombo vya kigeni… Kwa baadhi, muungano tawala, unaoundwa na vyama vilivyoainishwa kama vyama vya mrengo wa kulia, uko tayari kubadilisha kwa kina Jamhuri ya Czech.

“Mashirika yasiyo ya kiserikali yanayolengwa na muswada huu yana hatari ya kufanyiwa unyanyasaji wa kiutawala ikiwa mamlaka itachagua hivyo,” anasema Katerina Safarikova, mwandishi wa safu ya habari wa tovuti ya habari Seznam Zpravy, akiongeza kuwa “hii inaathiri idadi kubwa ya watu, kwani sheria hii inahusu kila aina ya mashirika yasiyo ya kiserikali, iwe katika misaada ya kibinadamu, afya ya akili, n.k.”

Kwa hivyo, umati mkubwa unatarajiwa katika maanamano ya leo, haswa kwa kuwa muswada huu wenye utata tayari umekosolewa na mkuu wa nchi, Petr Pavel, ambaye Wacheki wengi walikuja kumuunga mkono mitaani mnamo Februari 1. Wanaounga mkono Umoja wa Ulaya (EU), wanaounga mkono Ukraine, na wanaounga mkono NATO, jenerali huyu wa zamani lazima sasa afanye kazi na serikali hii yenye uhasama wa waziwazi … na haswa na Waziri Mkuu Andrej Babiš, ambaye tayari ametangaza nia yake ya kumtimua kwenye nafasi yake na kuteua mtu mwengine atakayechukuwa nafasi hiyo katika mkutano ujao wa NATO mwezi Julai.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *