Kamandi Kuu ya Jeshi la Marekani (CENTCOM) imesema kuwa imekamata meli ya mizigo yenye bendera ya Iran iliyokuwa ikijaribu kukwepa marufuku iliyowekwa kwa meli zote zinazoingia au kutoka katika bandari za Iran.

CENTCOM ilisema meli hiyo ilikamatwa Jumanne baada ya kuondoka katika mji wa bandari wa Bandar Abbas na kupita katika Mlango-Bahari wa Hormuz.

Pia iliongeza kuwa meli ya Jeshi la Wanamaji la Marekani, USS Spruance, ilifanikiwa kuigeuza mwelekeo meli hiyo, ambayo sasa inarejea Iran.

CENTCOM ilisema pia kuwa imezirudisha nyuma meli 10 kuelekea Iran, na kwamba hakuna meli iliyokiuka zuio hilo tangu lilipoanza kutekelezwa Jumatatu.

#StarTvUpdate
#chanzobbcswahili

(Feed generated with FetchRSS)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *