
Uzinduzi wa taratibu wa taasisi zinazotokana na uchaguzi wa hivi karibuni wa wabunge unaanza leo Jumatatu, Mei 4. Baada ya miaka mitano wakihudumu, wabunge wa bunge la saba walikamilisha rasmi misheni yao Aprili 30.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Na mwandishi wetu huko Bangui, Rolf Steve Domia-leu
Rais Faustin-Archange Touadéra amewaita wabunge waliochaguliwa wa bunge la nane kwa kikao cha kipekee kuanzia Mei 4 hadi 18, baada ya uchaguzi mkuu mwezi Desemba mwaka uliyopita. Hata hivyo, kikao hiki cha bunge kinafanyika katika muktadha wa wa kipekee huku Bunge la taifa likiwa halijakamilika.
Kikao hiki kisichokuwa cha kawaida kitajadili hatua muhimu: kuwekwa kwa wabunge, uzinduzi wa ofisi ya Bunge la taifa, na uundaji wa kamati za kudumu na makundi ya wabunge. Hata hivyo, orodha bado haijakamilika. Kati ya viti 144 katika Bunge la taifa, ni wabunge 90 pekee watakaowekwa wakati litakapofunguliwa leo Jumatatu, Mei 4, 2026.
Kusubiri
Chama tawala kinashikilia takriban viti hamsini, huku vilivyobaki vikishirikiwa kati ya wagombea huru na vyama vya siasa. Ikumbukwe pia kwamba upinzani ulichagua kususia uchaguzi huu. Viti vingine 54 bado vinasubiri, vimesitishwa kutokana na matokeo ya duru ya pili yanayoendelea hivi sasa katika majimbo kadhaa, ambayo baadhi yake yanapigiwa kura kwa sehemu.
Maswali
Hali hii inaibua maswali kuhusu uwakilishi wa bunge jipya. Hta hivyo, baadhi ya wajumbe wa serikali, waliochaguliwa kama wabunge, bado wanashikilia nafasi zao za uwaziri, kinyume na sheria zilizoainishwa na Katiba ya Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR). Katika ngazi ya urais, mabadiliko ya serikali yanatarajiwa baada ya kutangazwa kwa matokeo ya mwisho. Hii inapaswa kufungua njia kwa timu mpya ya utendaji na simamii wa nchi.