Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa amekosoa hali ya kisiasa nchini Sudan Kusini mbele ya Baraza la Usalama. Sudan Kusini inatarajia kufanya uchaguzi wake wa kwanza kabisa. Tangu uhuru wake mwaka wa 2011, Sudan Kusini imekuwa ikikumbwa na mfululizo wa migogoro mibaya.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Katika wiki za hivi karibuni, mapigano yameongezeka kati ya vikosi vya serikali vinavyomtii Rais Salva Kiir na wanamgambo wa upinzani wanaomtii Riek Machar, makamu wa rais ambaye amesimamishwa kazi na kupewa kifungo cha nyumbani kwa mwaka mmoja.

Marekani inatishia kuondoa ufadhili wake kwa ajili ya uchaguzi uliopangwa kufanyika mwezi Desemba 2026 nchini Sudan Kusini. Mwishoni mwa mwezi Aprili, Juba ilithibitisha azimio lake la kufanya uchaguzi huu, wa kwanza katika historia ya nchi hiyo tangu uhuru wake mwaka wa 2011.

Lakini kwa Washington, kuna masharti: hasa kuachiliwa kwa wafungwa wa kisiasa na kufanyika kwa mazungumzo na upinzani nchini humo, nchi ambayo sasa inachukuliwa na Umoja wa Mataifa kuwa karibu na vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Ni balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa aliyetoa onyo hili. Mbele ya Baraza la Usalama, Mike Waltz ameonyesha shaka kuhusu uwezekano wa kufanya uchaguzi unaoaminika nchini Sudan Kusini. Washington inasema hakuwezi kuwa na uchaguzi “huru na wa haki” bila kwanza kufanya mazungumzo ya kweli ya kisiasa. Mazungumzo kama hayo hayawezekani mradi tu “viongozi muhimu wamefungwa,” akiwemo Riek Machar, mkuu wa chama cha pili kwa ukubwa, moja waya vyama na mashirika ya kiraia waliotia saini makubaliano ya amani ya 2018.

“Hakuna” dalili ya kuanza kwa maandalizi 

Marekani pia inasikitishwa kuona “hakuna” maandalizi. Lakini, wanasema, hakuna swali la wafadhili wa kigeni kulipia mchakato ambao serikali ya Sudan Kusini haijifadhili yenyewe.

Kulingana na mtafiti Emmanuelle Veuillet, mwanafunzi katika chuo kikuu, hivyo Marekani inajaribu kutoa shinikizo la kuisukuma Juba kutekeleza makubaliano ya amani, ambayo ilitaja sensa mpya kama sharti la uchaguzi, na kuanzisha sheria ya uchaguzi na katiba. Hata hivyo, hakuna hata moja kati ya haya ambayo yamefanyika.

Athari ya tishio la Marekani itakuwa nini? Mtafiti hafuti uwezekano kwamba Sudan Kusini itawageukia washirika wengine kufadhili chaguzi hizi au kukubali uchaguzi mdogo, “wa kulazimishwa”.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *