Australia imejitolea kwa misheni ya “isiyo na upande wowote na ya amani” iliyopendekezwa na Ufaransa na Uingereza ili kulinda Mlango-Bahari wa Hormuz, Waziri wa Ulinzi Richard Marles amesema leo Jumatano.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Na: RFI na mashirika mengine

Matangazo ya kibiashara

Australia iko tayari kuunga mkono misheni huru, ya ulinzi mkali, wa kijeshi wa kimataifa, unayoongozwa na Uingereza na Ufaransa, mara tu itakapoanzishwa,” Marles amesema katika taarifa.

Canberra itaipa misheni hiyo ndege ya ufuatiliaji ya E-7A Wedgetail, ambayo tayari imetumwa katika eneo hilo kulinda Falme za Kiarabu kutokana na mashambulizi ya ndege zisizo na rubani za Iran, Marles amesema baada ya mkutano kwa njia y video kuhusu mada hiyo na wenzake kutoka nchi zipatazo 40.

Misheni hii ya kijeshi ya kimataifa italenga kukamilisha juhudi za kidiplomasia na hatua za kupunguza mvutano, huku “ikionyesha kujitolea kwa usalama wa biashara ya kimataifa,” waziri wa Australia ameongeza.

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron alitangaza “mpango ujao katika Umoja wa Mataifa” wa kupendekeza “mfumo” wa misheni hii ya baadaye, ambayo inatarajiwa kuanza mara tu Iran na Marekani zitakapokubaliana kuondoa vikwazo vyao, na kwa kushauriana na nchi hizi mbili.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *