Mali: Je, vita dhidi ya ugaidi inahalalisha utekaji nyara na usalama wa taifaMali: Je, vita dhidi ya ugaidi inahalalisha utekaji nyara na usalama wa taifa

Nchini Mali, hakuna habari za wakili na mwanasiasa Mountaga Tall kwa karibu wiki tatu. Baada yake, watetezi wengine wa demokrasia na ndugu wa wanachama wa upinzani walio uhamishoni wametekwa nyara na watu wenye silaha na waliojifunika nyuso zao, mfumo wa kawaida wa Usalama wa Taifa. Wote wanashikiliwa katika maeneo yasiyojulikana, nje ya mchakato wowote wa kisheria.

Imechapishwa:

Dakika 3 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Mtoto wa Mountaga Tall, wanajeshi, na maafisa kutoka shule za Quran pia wametoweka. Hakuna taarifa rasmi iliyotolewa na mamlaka kuhusu mahali walipo. Mnamo Mei 1, mahakama ya kijeshi ilibaini kwamba ilikuwa inawachunguza watu wanaoshukiwa kushiriki katika mashambulizi ya Aprili 25, yaliyofanywa na wanajihadi wa JNIM na waasi wa FLA. Je, haja ya kuchunguza mitandao inayoshukiwa ya kigaidi na mahitaji ya asili ya uchunguzi kama huo yanahalalisha vitendo hivi?

Familia za watu hao waliotoweka zinaendelea kuwa na wasiwasi, zikiuliza wapendwa wao wanashikiliwa wapi, katika mazingira gani, na kwa sheria gani. Zaidi ya yote, wanadai kwamba, ikiwa wanashutumiwa kwa makosa yoyote, kesi zao zipelekwe mahakamani. Lakini kwa wafuasi wa mamlaka ya mpito, maslahi ya juu ya serikali na mapambano dhidi ya ugaidi vinahalalisha mbinu hiyo.

Maslahi ya kitaifa

“Kuna uchunguzi uliofanywa na ofisi ya mwendesha mashtaka katika mahakama ya kijeshi, ambao unahitaji uwezo wa kipekee,” anasema Tiambel Guimbayara, mwandishi wa habari wa Mali, mhariri wa La Voix du Mali, na mfuasi na mawanaharakati wa serikali ya sasa. ” Maslahi ya kitaifa yanaruhusu uchunguzi wowote unaohitajika kwa usalama wa taifa. Baada ya yote, mashambulizi ya Aprili 25 yalihusisha kifo cha Waziri wa Ulinzi, Jenerali Sadio Camara, mmoja wa watu muhimu zaidi katika utawala uliopo! Ninaamini kwamba maslahi ya taifa yanapewa kipaumbele kuliko kila kitu, haswa katika hali za kipekee, haswa wakati wa kukabiliana na makundi ya kigaidi na ugaidi kwa ujumla.”

“Ili Serikali isipoteze nafasi yake” 

Kauli hii inapingana na Katiba ya Mali, pamoja na Sheria ya Kimataifa ya Haki za Kiraia na Kisiasa na Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Watu. Nakala hizi mbili, ambazoo Mali ilitia saini, zinafafanua usawa kati ya haki ya Serikali ya kujilinda na wajibu wake wa kuwalinda raia wake. Hivi ndivyo Jean-François Akandji-Kombé, profesa katika Chuo Kikuu cha Sorbonne na mtaalamu wa sheria za kimataifa na z kijaamii barani Afrika, anavyokumbusha

“Serikali y a Mali ina kila haki ya kulinda taifa la Mali dhidi ya ugaidi,” anasema Profesa Akandji-Kombé, “lakini kwa ajili ya ulinzi wa jamii ya Mali yenyewe, taifa la Mali halipaswi kusimamisha utekelezaji wa uhuru wote na, katika masuala ya mashtaka, haki ya jaji, haki ya kudhaniwa kutokuwa na hatia, au haki ya kutetewa na wakili. Haki hizi haziwezi kukandamizwa. Ni vipengele muhimu vya kudumisha mshikamano wa jamii, kwa ajili ya kuhakikisha kwamba taifa halipotezi nafasi yake katika mapambano dhidi ya ugaidi, dhidi ya hatari zote zinazoweza kutishia maisha ya taifa.”

Wachunguzi wengi wanabaini kwamba utawala unatumia kisingizio cha mashambulizi ya Aprili 25 na msako wa washirika watarajiwa ili kuwaondoa wapinzani wa kisiasa waliojitolea kwa demokrasia.

Visa vingi vya utekaji nyara ambavyo vimetokea katika wiki tatu zilizopita havijaripotiwa na mamlaka ya mpito.

Kundi la mawakili wanaowakilisha familia ya mwanasheria Mountaga Tall walitoa taarifa siku ya Jumanne wakielezea “kusikitishwa kwao” kufuatia kutoweka kwa mtoto wa mwenzao, Cheikh Mamadou Tall mnamo Mei 16. Kundi hilo linatoa wito kwa “mamlaka husika za utawala na mahakama kufanya kila liwezekanalo ili kuhakikisha kuachiliwa kwa watu wote hao wawili na kutoa mwanga kuhusu mazingira ya kutoweka kwao.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *