Rwanda imejibu kauli za Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio, ambaye aliikosoa Kigali kwa kushindwa kuheshimu makubaliano ya amani yaliyosainiwa Washington kuhusu mgogoro mashariki mwa DRC. Marekani pia ilweka vikwazo kwa jeshi la Rwanda kwa kuunga mkono kundi la kisiasa na kijeshi la AFC/M23.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Na mwandishi wetu mjini Kigali, Lucie Mouillaud

Kigali imepokea kauli za Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, ikiwa ni pamoja na kutambua kwake juhudi za Rwanda za kuheshimu ahadi zake katika makubaliano ya amani ya Washington.

Akihojiwa mbele ya kamati ya Baraza la Wawakilishi wiki hii, Marco Rubio alisema kwamba anaona “kwamba mambo yanaendelea” na anatumai kuondolewa kwa wanajeshi wa Rwanda kutoka mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ifikapo “katikati ya mwezi ujao.”

Katika taarifa, Kigali ilijibu, ikidai kwamba pande zote lazima ziheshimu ahadi zao. Katika taarifa yake, Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda Olivier Nduhungirehe aliishutumu Kinshasa kwa “ukiukwaji mkubwa” wa makubaliano na kushutumu “uungaji mkono unaoendelea kutoka kwa serikali ya Kongo kwa kundi lenye silaha la FDLR (waasi wa Rwanda), pamoja na mashambulizi ya ndege zisizo na rubani katika maeneo ya raia.” “Makubaliano haya hayawezi kutumika kwa njia ya kuchagua, na majukumu ya kila upande hayawezi kutenganishwa,” Rwanda ilibainisha, ikiongeza kwamba “upendeleo hauwezi kutatua tatizo.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *