
Iran inachapisha mwongozo wa kutoza meli za mizigo zinazopita kwenye mlango wa Bahari ya Hormuz kwa ajili ya usalama wa bahari na huduma ya mazingira.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Makalu wa rais wa Iran Shina Ansari, anayehusika na maswala ya Mazingira, amesema mwongozo huo unaelekea kukamilika.
Hata hivyo, kiwango cha ada na namna wa ukusanyaji wa makato hayo, hakijafahamika, wakati huu mchakato wa mwongozo huo ukiendelea kabla ya kuwasilisha kwa wahusika.
Ansari, amesema mlango wa Bahari wa Hormuz, unaangukia kwenye eneo la utozwaji wa k kodi, inayopakana na nchi za Iran na Oman.