
TABORA; Kamandawa Polisi Mkoa wa Tabora (RPC), Richard Abwao amefariki dunia leo Juni 20, 2026 akiwa kwenye matibabu Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paul Chacha amesema Kamanda Abwao alikuwa akipatiwa matibabu kwenye hospitali hiyo, lakini leo wamepokea taarifa hizo za kusikitisha.
Amemueleze hayati Avwao kama kiongozi shupavu aliyepambana kwa nguvu zote dhidi ya vitendo vya uhalifu mkoani Tabora, akibainisha kuwa mchango wake katika kuimarisha usalama wa wananchi utaendelea kukumbukwa.