#HABARI: Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) upande wa Zanzibar, Said Mzee Said ameliomba Jeshi la Polisi kuwaachia huru wafuasi wa chama hicho wanaoshikiliwa kwa tuhuma za kuhamasisha maandamano yanayodaiwa kupangwa kufanyika Julai 7, 2026.
Akizungumza Juni 19, 2026, wakati akihutubia wananchi katika Kata ya Chinongwe iliyopo Mkoani Lindi, Said Mzee amesisitiza kuwa CHADEMA haihusiki kwa namna yoyote na mipango ya maandamano hayo kama inavyodhaniwa na vyombo vya ulinzi na usalama.
Amebainisha kuwa amepokea taarifa za kukamatwa kwa makada sita wa chama hicho na akatumia fursa hiyo kuwatoa hofu Watanzania kuhusu msimamo wa chama.
Kwa taarifa zaidi ufuate (follow) ukurasa wetu mpya wa Facebook #ITV EXTRA>>>> https://www.facebook.com/share/1QMjXDHqGv/?mibextid=wwXIfr
Powered by #MCHEZOSUPA
JINSI YA KUSHIRIKI MCHEZO SUPA:
-
Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M – Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.
#ITVDigital #ITVUpdates ITVTanzania
Follow ITV TANZANIA RadioOne Tanzania
Capitalradio Tanzania
(Feed generated with FetchRSS)