
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Qatar imesema kwamba kiwango cha vitisho vya usalama nchini ni cha juu na imewasihi kila raia wake kubaki nyumbani au kuwa katika maeneo salama. Wizara hiyo imewataka raia kuzingatia miongozo ya usalama na kuepuka safari zisizo za lazima.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Qatar iliwasihi wakazi kubaki majumbani mwao, kuepuka kutoka nje, na kukaa mbali na madirisha na nafasi wazi, kulingana na shirika la habari la Qatar.
Tahadhari hii ilifuatia tangazo la Kuwait kwamba ulinzi wake wa anga ulikuwa chini ya mashambulizi ya makombora na ndege zisizo na rubani, huku Bahrain ikiwasha ving’ora vyake kufuatia mashambulizi ya anga na kuwasihi raia wake na wakazi wake kutafuta hifadhi katika eneo salama.
Hatua hizi za dharura zinakuja kufuatia wimbi jipya la mashambulizi ya anga ya Marekani dhidi ya Iran na mashambulizi ya kulipiza kisasi ya Iran katika Ghuba.
Kulingana na ripoti, Marekani ilifanya mashambulizi mapya dhidi ya Iran mnamo Julai 8 baada ya mashambulizi dhidi ya meli za kibiashara katika Mlango-Bahari wa Hormuz, huku Iran ikilenga kmbi za jeshi la Marekani huko Bahrain na Kuwait kwa kulipiza kisasi.
Wakati huo huo mataifa ya Ghuba hivi karibuni yalikitoa tahadhari za dharura kufuatia kuongezeka kwa mvutano kati ya Marekani na Iran.