Mawakili wanaowawakilisha waathiriwa wa utekaji nyara na mauaji, pamoja na mashirika ya kiraia nchini DRC, waliwasilisha malalamiko kwa Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Shirikisho la Ubelgiji siku ya Ijumaa, Julai 10, 2026, na pia “Mawasiliano chini ya Kifungu cha 15,” sawa na malalamiko kwa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu huko Hague.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Na mwandishi wetu mjini Brussels, Pierre Bénazet

Malalamiko kuhusu sula hili yaliwasilishwa mwaka mmoja uliopita mjini Brussels dhidi ya watu tisa wa familia ya Félix Tshisekedi. Hatimaye, kesi kuhusu uporaji huu uko katika mfumo wa haki.

Malalamiko hayo yanadai uhalifu dhidi ya ubinadamu, ambao walalamikaji wanadai umekuwa ukifanywa mara kwa mara kwa miaka sita iliyopita dhidi ya wale wanaopinga familia ya rais kudhibiti rasilimali za madini za Katanga.

Kesi kumi na moja zawekwa mbele

Wanasheria wanalaani matukio kumi na moja ambapo uhalifu dhidi ya ubinadamu umerekodiwa, kama vile mamia ya vifo na majeraha mwaka wa 2024 katika gereza la Makala mjini Kinshasa na mauaji kadhaa huko Lubumbashi, Kolwezi, na kwingineko huko Katanga.

Kulingana na wakili Hervé Diakiese, ukandamizaji huo unategemea MSU (Kitengo cha Usalama wa Kijeshi), wanamgambo wa Force du Progrès wa chama tawala, UDPS, na wanachama wa kabila la Rais Félix Tshisekedi: “Kumekuwa na matamshi yaliyotolewa na mamlaka za utawala na zile zilizopewa mamlaka ya serikali, zikidai kwamba Waluba, kama wanavyowatambua, kwa kweli, watu wa Kasai, hawana mamlaka tu, “bali wao ni mamlaka.”

Na kwa wakili Bernard Maingain, mfumo wa haki wa Kongo unashindwa kufanya kazi yake  kutokana na ukandamizaji: “Tuko katika hali hii ya kushindwa kwa mahakama nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, na tunasikitika. Masharti ya kufanya kile kinachoitwa ‘mawasiliano, Kifungu cha 15’ cha Mkataba wa Roma yametimizwa kikamilifu. Marejeleo yanafanywa na mawakili, na hakuna anayeweza kuyapinga. Hakuna anayeweza kutangaza kuwa hayakubaliki.”

Sasa inabaki kwa waendesha mashtaka huko Brussels na Hague kuamua kama watafungua uchunguzi au la.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *