DAR ES SALAAM: Maonesho ya kimataifa ya Africa Agri Expo yanatarajiwa kurejea kwa mara nyingine kwa kuadhimisha toleo lake la 10, ambapo yataambatana na maonesho ya Future Food Livestock & Poultry Expo yatakayofanyika Septemba 2 hadi 3, 2026 jijini Dar es Salaam, na litawakutanisha wadau wa sekta za kilimo, mifugo, biashara ya kilimo, uwekezaji na ubunifu kutoka barani Afrika na sehemu mbalimbali duniani.
Katika maonesho hayo, washiriki watapata fursa ya kujifunza na kujionea teknolojia za kisasa za kilimo, mifumo ya umwagiliaji, mashine za kisasa za kilimo, pamoja na suluhisho mbalimbali kwa sekta za mifugo. Pia kutakuwa na mijadala kuhusu usalama wa chakula, kilimo kinachokabiliana na mabadiliko ya tabianchi, na fursa za uwekezaji katika sekta nzima ya kilimo.
Africa Agri Expo 2026 itatoa nafasi kwa kampuni na taasisi mbalimbali kuonesha bidhaa na huduma zao, kujenga ushirikiano wa kimkakati wa kibiashara, kuunganishwa na wanunuzi, wasambazaji na wawekezaji, pamoja na kuimarisha uwepo wao katika moja ya masoko ya kilimo yanayokua kwa kasi zaidi duniani.
Afrika ina zaidi ya asilimia 60 ya ardhi yenye rutuba ambayo bado haijalimwa duniani, hali inayolifanya bara hilo kuwa kitovu cha fursa mpya za uwekezaji na biashara ya kilimo. Tanzania, kutokana na nafasi yake ya kimkakati na ukuaji wa kasi wa sekta ya kilimo, imeendelea kuwa lango muhimu kwa wawekezaji na wafanyabiashara wanaolenga masoko ya Afrika Mashariki na Kati.
Usikose fursa hii. Jiunge na maelfu ya wadau wa sekta ya kilimo katika maonesho hayo makubwa ya biashara ya kilimo barani Afrika. Jisajili leo, shiriki kama mtoa maonesho, mdhamini au mshirika, na uwe sehemu ya kuchagiza mustakabali wa kilimo, usalama wa chakula na biashara ya kilimo barani Afrika.
