Nchini Sudan, baada ya miezi kadhaa ya kuzingirwa, hali ni mbaya kwa wakazi wa jiji la Sudan la El-Obeid, njia panda ya kimkakati huko Kordofan Kusini, iliyozingirwa na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vya Jenerali Mohamed Hamdane Dogolo, anayejulikana kama “Hemedti.” 

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) linaelezea wasiwasi wake. Idadi ya wakazi nusu milioni katika jiji hilo imeongezeka kwa kasi kutokana na kuongezeka kwa watu waliokimbia makazi yao, na uhaba wa bidhaa za msingi unazidisha hali hiyo.

Kwa miezi kadhaa, Mji wa El-Obeid nchini Sudan umekuwa ukizingirwa kwa kiasi na wanamgambo wa RSF, ambao hushambulia jiji na maeneo jirani mara kwa mara. Matokeo yake, bei za chakula zimepanda mara dufu.

“Baadhi ya viungo vya msingi vya kupikia, kama vile mafuta, vitunguu, sukari, na chai, vimekuwa vigumu kununua. Kwa mfano, sukari imepanda kutoka pauni za Sudan 3,000 hadi 8,000. Familia nyingi haziwezi tena kumudu kununua vya kutosha na zinakula mara moja tu kwa siku,” anaelezea Usra, mkazi wa El-Obeid, akizungumza na Alexandra Brangeon wa kitengo cha RFI kanda ya Afrika.

Hivi ndivyo ilivyo kwa maji, anasema Duaa Tariq, mwanachama wa mtandao wa misaada ya kijamii. Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) wanashambulia kwa makusudi malori yanayobeba bidhaa kwa ajili ya kusambaza mjini, ili kuzuia wafanyabiashara na kusababisha uhaba, anaelezea.

“Unapokaribia El-Obeid, unaweza kuona malori yaliyoharibiwa kando ya barabara, pamoja na magari ya kijeshi, hakuna mabasi yanayosafiri. Yanalengwa na mashambulizi ya RSF. Na katika jiji lenyewe, vituo vya mafuta, vituo vya kusukuma maji, na mitambo ya umeme vimeshambuliwa ili kusababisha uhaba … Kumbuka, huko Khartoum na El-Fasher, njaa ilisababishwa na kufungwa kwa masoko.”

Hali hii ya kibinadamu inazidishwa na idadi inayoongezeka ya watu waliokimbia makazi yao wanaofika kila siku El-Obeid, inayokadiriwa kuwa zaidi ya 100,000.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *