Hii inamaanisha kuanzia mwaka ujao wanafunzi kutoka Israel hawatokubaliwa kujiunga na chuo hicho kinachotoa mafunzo ya kimataifa ya kimkakati kwa wanafunzi wa Uingereza na maeneo mengine ya dunia.

Israel imekasirishwa na uamuzi huo iliyouita wa kibaguzi unaokwenda kinyume na tamaduni za Uingereza za uvumilivu, utu na uadilifu.

Ingawa Uingereza inabakia kuwa mshirika wa karibu wa Israel, lakini hivi karibuni imekuwa ikiishinikiza nchi hiyo kuachana na vita vyake huko Gaza, ikitishia mwezi Julai kuitambua Palestina kama dola huru iwapo Israel haitochukua hatua za kupunguza operesheni zake huko.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *