Daktari mmoja mwandamizi katika Hospitali ya umma Karachi aliiambia BBC News kwamba miili tisa na takribani watu 32 waliojeruhiwa walipelekwa hospitalini baada ya mapigano makali na polisi karibu na ofisi ya kibalozi ya Marekani mjini Karachi.
Mamia ya waandamanaji wanaoiunga mkono Iran waliingia barabarani katika miji ya Karachi, Lahore na Islamabad kufuatia mashambulizi ya Marekani na Israel dhidi ya Iran.
Afisa wa Edhi Foundation, huduma binafsi ya uokoaji, pia alithibitisha kuwa walipeleka miili tisa ya watu waliokufa na makumi ya waliojeruhiwa hospitalini.
Mapigano yalianza wakati polisi walipojaribu kuwazuia waandamanaji kuingia katika eneo la ubalozi huo. Polisi bado hawajatoa taarifa rasmi kuhusu hali hiyo.
Afisa mmoja wa Umoja wa Mataifa, aliiambia BBC News kwamba ofisi ya Umoja wa Mataifa ilichomwa moto huko Gilgit, katika eneo la Gilgit-Baltistan linalosimamiwa na Pakistan.
Polisi walithibitisha kuwa amri ya kutotoka nje iliwekwa katika eneo hilo baada ya mamia ya watu kuanza maandamano.
Mashirika ya Washia yalikuwa yametangaza maandamano katika miji kadhaa, ikiwemo Islamabad.
#StarTvUpdate
#chanzobbcswahili

(Feed generated with FetchRSS)