
Marekani imeidhinisha kwa muda uuzaji wa mafuta ya Urusi yaliyohifadhiwa kwenye meli, huku bei zikipanda tangu kuanza kwa vita vya Iran, Wizara ya Fedha ya Marekani imetangaza siku ya Alhamisi.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Wizara hiyo imetoa leseni inayoidhinisha uuzaji wa mafuta ghafi ya Urusi na bidhaa za petroli zilizopakiwa kwenye meli hadi Aprili 11 kabla ya Machi 12 saa 12:01 usiku.
Wizara ya fedha ya Marekani imetoa tangazo hilo jana ikiidhinisha usafirishaji na uuzaji wa mafuta ghafi ya Urusi na bidhaa nyingine za petroli zilizokwama baharini. Waziri wa fedha wa Marekani, Scott Bessent, alisema idhini hiyo mpya inalenga kuongeza uwiano wa kimataifa wa upatikanaji mafuta yaliyopo, lakini akisisitiza kuwa hizo ni hatua za muda mfupi.
Hatua hiyo inamaanisha kulegeza kwa muda vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Urusi, nchi ambayo imelengwa kutokana na uvamizi wake nchini Ukraine.
Mashambulizi ya Marekani na Israel dhidi ya Iran yamelitumbukiza eneo la Mashariki ya Kati vitani.