Kulingana na makala ya Axios iliyochapishwa siku ya Jumapili, ikimnukuu afisa wa Marekani na vyanzo viwili vinavyofahamu jambo hilo, Iran imewasilisha pendekezo jipya kwa Marekani, kupitia wapatanishi wa Pakistan, linalolenga kufungua tena Mlango-Bahari wa Hormuz na kukomesha vita, huku mazungumzo ya nyuklia yakiahirishwa hadi tarehe itakayotangazwa.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Na: RFI na mashirika mengine

Matangazo ya kibiashara

Makala hiyo pia inasema kwamba Rais wa Marekani Donald Trump anatarajiwa kufanya mkutano wa dharura na timu yake ya usalama wa taifa na sera za kigeni ili kutathmini hatua zinazowezekana kuchukua.

Ombi hili  la Iran linahusisha kuondolewa kwa kizuizi cha kijeshi kwa mali za Iran zinazopitia kwenye mlango-bahari, uwezo pekee ambao Marekani inao juu ya utawala wa Iran katika muktadha wa mazungumzo ya makubaliano ya nyuklia.

Siku ya Jumapili, Trump alionyesha nia yake ya kudumisha kizuizi hicho hadi makubaliano kamili na utawala wa Iran yatakapofikiwa.

“Wakati kiasi kikubwa cha mafuta kinapita kwenye mfumo wako … ikiwa, kwa sababu moja au nyingine, bomba hilo litafungwa kwa sababu haliwezi kuwekwa kwenye makontena au kusafirishwa kwa meli … kinachotokea ni bomba kulipuka kutoka ndani … wanasema wana siku tatu tu kabla ya hilo kutokea,” Trump aliambia Fox News siku ya Jumapili.

“Na linapolipuka, huwezi kulijenga tena sawasawa … litakuwa asilimia 50 tu ya uwezo wake wa sasa. Kwa hivyo nadhani wako chini ya shinikizo,” aliongeza.

Araghchi anasema mazungumzo na Oman yanalenga kuhakikisha urambazaji salama katika Mlango-Bahari wa Hormuz.

Mapema Jumapili jioni, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi aliondoka Oman baada ya ziara nchini humo kwa “mazungumzo ya pande mbili,” akiishukuru serikali ya Oman kwa “namna ilibyowapokea.”

“Majirani zetu ndio kipaumbele chetu,” alisema.

Matamshi ya Araghchi yanakuja anapoondoka kwenda Moscow kwa mfululizo wa mazungumzo na washirika wa kikanda, yanayoendelea sambamba na mazungumzo na Marekani. Kabla ya kusafiri kwenda Oman, alikutana na maafisa wa Pakistan huko Islamabad.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *