Kundi la waasi  wa AFC/M23 limejiondoa Jumanne, Mei 12, na kupiga kambi umbali wa zaidi ya kilomita 70 kutoka Uvira, jiji lililoko mashariki mwa nchi ambalo ilikuwa imelikalia kwa muda mfupi mnamo mwezi Desemba 2015. Kwa kujiondoa huku, hatua ya kwanza muhimu tangu kutekwa kwa jiji hilo, AFC/M23 inayoungwa mkono na Rwanda inakubali shinikizo kutoka Washington, ambayo ilikasirishwa na kuingia kwake Uvira licha ya makubaliano ya amani.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Baada ya kujiondoa kwa mara ya kwanza Jumatatu, Mei 11, kutoka Sange hadi Luvungi, wapiganaji wa AFC/M23 waliendelea na kujiondoa katika maeneo mbalimbali siku ya Jumanne, Mei 12, kando ya barabara ya Uvira-Bukavu, na kwa sasa wamepiga kambi katika mji wa Kamanyola, kilomita 70 kaskazini mwa Uvira. Baada ya hapo, jeshi la DRC lilitangaza kuingia katika mji wa Luvungi na maeneo ya uwanda wa Ruzizi na Nyanda za Juu, maeneo yaliyoachwa na kundi hilo lenye silaha.

Kujiondoa huku ni matokeo ya shinikizo la kijeshi na kidiplomasia, kulingana na Luteni Reagan Mbuyi, msemaji wa jeshi la Kongo huko Kivu Kusini. AFC/M23 iliifanya Washington inakupatwa na hasira kwa kuingia Uvira mnamo mwezi Desemba 2025. Mwakilishi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa kisha akataka kundi hilo liondoke kabisa na kwenda umbali wa angalau kilomita 75 kutoka jiji hilo na kuzingatia majukumu yake chini ya makubaliano ya amani. Tangu wakati huo, Washington pia imeweka vikwazo kwa jeshi la Rwanda na maafisa kadhaa wa serikali.

Kwa upande wake, AFC/M23 haizungumzii kujiondoa bali kujipanga upya. Hii inaonekana kama ishara ya nia njema ndani ya mchakato wa amani, kulingana na afisa mkuu wa kundi hilo. Siku ya Jumanne jioni, msemaji wa Jeshi la Kongo huko Kivu Kusini alidai kwamba Rwanda ilikuwa imeweka silaha nzito kwenye vilima vilivyo upande wake wa mpaka, ili kudumisha udhibiti wa kijeshi katika eneo la Kamanyola na viunga vyake.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *