Baada ya mkutano wa kilele wa Afrika na Ufaransa jijini Nairobi, Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron alielekea nchini Ethiopia Jumatano wiki hii na kuwa na mkutano usio wa kawaida na Rais wa Tume ya Afrika Mahmoud Ali Youssouf na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres, rais wa Ufaransa aliendelea kutetea sauti yenye nguvu zaidi ya kimataifa kwa Afrika.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Emmanuel Macron ametoa wito wa utekelezaji wa Azimio la Umoja wa Mataifa nambari 27-19, Lililopitishwa mwishoni mwa 2023, linazilazimisha nchi wanachama kufadhili shughuli za amani za AU.

‘‘Azimio hili bado halijapata matumizi ya moja kwa moja na halisi kwa sababu limekwama. Kwa hivyo, sisi watatu tumejitolea kweli kusukuma suala hili mbele na kutekeleza azimio hili muhimu. Ni chombo pana, chenye nguvu, na kinachoaminika, ambacho, zaidi ya hayo, kinaonyesha kwamba ushirikiano wa pande nyingi hufanya kazi wakati rasilimali muhimu zinapotengwa.’’ Amesema Rais Macron.

Katibu Mkuu wa UN akiwa na Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika nchini Ethiopia Jumatano 13.05.26
Katibu Mkuu wa UN akiwa na Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika nchini Ethiopia Jumatano 13.05.26 AP – Amanuel Sileshi

Rais wa Ufaransa pia alisisitiza uungwaji mkono wake kwa uwakilishi wa Afrika katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

‘‘Tunapigania Afrika iwakilishwe miongoni mwa wanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama. Nilimwambia Rais: ikiwa mwanachama mmoja au wawili wangeteuliwa mahususi na Umoja wa Afrika, kwa makubaliano ya wanachama wote, nina uhakika kwamba hakuna hata mmoja wa wanachama wa kudumu ambaye angeweza kuzuia hilo. Kwa vyovyote vile, tutafanya kazi yote ya kidiplomasia pamoja nawe. Lakini wakati umefika.’’ Amesisitiza Rais Macron.

Siku ya Jumatano, Emmanuel Macron pia alikutana na Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed. Wawili hao, ambao wamekuwa na urafiki mkubwa tangu mkutano wao wa kwanza mwaka wa 2019, walijadili, miongoni mwa mambo mengine, ushirikiano wa kiuchumi kati ya nchi zao mbili.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *