Mafanikio Serengeti Boys yatinga bungeniMafanikio Serengeti Boys yatinga bungeni

DODOMA; MBUNGE wa Bunda Mjini, Amos Bulaya muda huu anawasilisha hoja bungeni kuhusu Azimio la Bunge kuipongeza timu ya Taifa ya Vijana chini ya umri wa miaka 17 (Serengeti Boys) kutinga hatua ya fainali katika michuano ya AFCON 2026 inayoendelea Morocco na kukata tiketi ya kushiriki Mashindano ya Kombe la Dunia la vijana chini ya umri huo mwaka 2026.

Serengeti Boys jana ilitinga fainali baada ya ushindi wa penalti 4-3 dhidi ya Misri kufuatia matokeo ya 0-0 baada ya dakika 90 za mchezo huo.

Hii ni mara ya kwanza kwa Tanzania kucheza fainali ya michuano hiyo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *