
Baada ya kufukuzwa kazi kwa Ousmane Sonko siku ya Ijumaa, Mei 22, 2026 na kuteuliwa kwa mrithi wake Ahmadou Al Aminou Mohamed Lô kama Waziri Mkuu mpya wa Senegal, tangazo la serikali mpya litaamua uwiano wa madaraka kati ya PASTEF na serikali katika siku zijazo.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Na mwandishi wetu huko Dakar, Pauline Le Troquier
Ni kitendo chenye usawa: rais wa Senegal atalazimika kukubali kuingia katika enzi mpya bila Ousmane Sonko kuwa upande wake huku pia akishirikiana na chama chake cha PASTEF. Kikiwa na viti 130 kati ya 165, chama cha PASTEF kina wingi wa viti katika Bunge la taifa. “Chama kina uwezo wa kumwajibisha Waziri Mkuu mpya, kwa mfano, kwa kuunda mazingira ya hoja ya kutokuwa na imani,” anabainisha Babacar Ndiaye, mchambuzi wa masuala ya siasa na mkurugenzi wa utafiti katika shirika la Think Thank Wathi.
Katika serikali ijayo ya Senegal, “lazima kutakuwa na mawaziri wa PASTEF,” chanzo ndani ya serikali inayoondoka kinatabiri. Na pamoja nao, kama Waziri Mkuu, chanzo hicho kinaongeza, “wataalamu wa ngazi ya juu waliobobea.”
“Ufafanuzi”
Bado haijabainika ikiwa watu kutoka kwa wasaidizi wa karibu wa Ousmane Sonko watakubali nafasi iliyotolewa na serikali kusimamia mradi huo. Wiki hii, chama cha PASTEF kiliweka masharti, kikianza na “ufafanuzi” kuhusu jinsi ya kulipa deni la nchi, linalokadiriwa kuwa 132% ya Pato la Taifa. Je, rais Bassirou Diomaye Faye atachagua marekebisho kama yale yaliyopendekezwa na IMF, chaguo ambalo kwa sasa linapingwa na chama cha Ousmane Sonko?
Mnamo Juni 6, 2026, katika mkutano mkuu wa kitaifa wa PASTEF, Ousmane Sonko atapata fursa ya kufafanua aina ya uhusiano wake na Mkuu wa Nchi na serikali mpya. Mzozo wa madaraka au ushirikiano? Kwa sasa, Bassirou Diomaye Faye hajajiuzulu wala kufukuzwa kutoka chama chake cha awali. Rais huyo wa Senegal alikuwa katika ziara ya kikazi jana huko Banjul, Gambia. Alirudi Dakar Jumamosi, Mei 30, saa 1:00 usiku.