
Afrika Kusini inasubiri kwa hamu siku ya Jumanne, Juni 30, 2026. Ingawa si tarehe rasmi, imechaguliwa na makundi yanayopinga uhamiaji haramu kudai kuondoka kwa wahamiaji wasio na vibali.
Imechapishwa:
Dakika 2 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Na mwandishi wetu nchini Afrika Kusini, Claire Bargelès
Siku ya Jumanne hii, Juni 30, maandamano yamepangwa kote Afrika Kusini, na ingawa mamlaka inasema iko tayari na waandaaji wanaahidi mikusanyiko ya amani, wahamiaji wana hofu ya kutokea machafuko mabaya na vurugu. Wanakumbuka maandamano ya chuki dhidi ya wageni ya mwaka 2008, ambayo yaligharimu maisha ya zaidi ya watu 60, pamoja na ghasia za mwaka 2021, zisizohusiana na masuala ya uhamiaji, ambazo zilisababisha vifo vya zaidi ya watu 350.
Katika kitongoji cha Yeoville, katikati mwa mji wa Johannesburg, mada hiyo inajitokeza katika kila mazungumzo miongoni mwa Wakongo wanaoishi nje ya nchi. Suzanne, akiwa amevaa kofia kubwa ya manyoya ili kujikinga na baridi, anauza matunda na mboga kando yabarabara yenye shughuli nyingi. Na anakasirika anaposikia Waafrika Kusini wakidai wahamiaji wasio na vibali warudi nyumbani kutatua matatizo ya nchi zao: “Niliondoka Kongo kwa sababu ya vita, kwa kuwa ninatoka mashariki, huko Kivu Kaskazini, katika eneo la Rutshuru. Nifanye nini? Nirudi wapi? Mahali ambapo hakuna amani?”
“Hawaelewi kwamba tuko vitani”
“Kwetu sisi Wakongo,” anaongeza, “hawaelewi kwamba tuko vitani. Tangu mwaka 2012, sijapata vibali vya kuishi hapa. Daima hunipa kibali cha kuishi tu mwaka, miezi sita.” Lakini ukienda kuomba kuongeza muda wa kuishi nchini Afrika Kusini, hakukubalii. Hawajanipa kibali chochote tangu mwezi Machi.”
Karibu na hapo, Feza anauza nguo za mitumba, ameketi kwenye kiti, akiota jua: “Hata watoto wana huzuni kwa sababu wanajua kwamba tarehe 30 tunapaswa kufukuzwa, tunapaswa kurudi Kongo. Hawajaijua Kongo tangu tulipofika; walizaliwa hapa. Tunaogopa sana. Kwa sababu watu hao hapa wanaweza kuwa wanatembea na mapanga na kila kitu; hatujui watafanya nini.”
“Nitaweka kufuli nyingi mlangoni”
“Kutokana na wasiwasi na baada ya kupitia vipindi zaidi vya vurugu za chuki dhidi ya wageni, Monda, mwanamuziki, anapanga kubaki nyumbani kwake: “Sijui kitakachotokea, lakini ikiwa mambo yataenda vibaya, sitatoka nje. Nitakaa nyumbani, nitajifungia ndani, nitaweka kufuli nyini mlangoni. Ndivyo ilivyo.”
Kulingana na serikali ya Afrika Kusini, DRC ni miongoni mwa nchi zinazotaka kuandaa zoezi la kurejesha kwa hiari raia wake, baada ya Ghana, Nigeria, Msumbiji, na Malawi. Kulingana na Waziri wa Sheria, katika wiki mbili zilizopita, zaidi ya raia 6,700 wa Malawi na karibu Wazimbabwe 1,500 tayari wamerejeshwa nyumbani kwa basi.