
Kiongozi wa upinzani nchini India Rahul Gandhi ametoa wito leo Jumanne, Julai 21, 2026, wa kujiuzulu kwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo Narendra Modi kufuatia kukandamizwa vibaya kwa maandamano ya wanafunzi yanayodai mageuzi katika mfumo wa vyuo vikuu na kufukuzwa kazi kwa waziri wa elimu.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Rahul Modi aapaswa kujiuzulu “kwa kuharibu mustakabali wa vijana wa India,” Gandhi, wa chama cha Congress, amesema katika ujumbe uliyorushwa kwenye mitandao ya kijamii wakati yeye na wabunge wengine wakitembea kwa mguu kuelekea makazi ya waziri mkuu huko New Delhi.
Siku ya Jumatatu, maelfu ya watu walikusanyika katika mji mkuu wa New Delhi kufuatia wito wa chama kinachoitisha maandamano hayo “chama cha mende” ambacho huunganisha hasira kuhusu udanganyifu wa mitihani na kutoridhika kwa vijana wa nchi hiyo.
Siku ya Jumatatu, maelfu ya watu walikusanyika katika mji mkuu, New Delhi, kwa wito wa harakati za maandamano ya Wahindi, “Chama cha Mende,” ambacho huunganisha hasira kuhusu udanganyifu wa mitihani na kutoridhika kwa vijana wa nchi hiyo.
Wakati wa maandamano haya, moja ya maandamano makubwa zaidi tangu Narendra Modi aingie madarakani mwaka wa 2014, angalau watu 180 walijeruhiwa kulingana na polisi, huku wanafunzi wakidai mamia walijeruhiwa baada ya polisi kufyatua gesi ya machozi na kuwapiga fimbo.
“Bw. Modi lazima ajiuzulu kwa kuharibu mustakabali wa vijana wa India,” alisema Rahul Gandhi wa chama cha Congress katika ujumbe uliyorushwa kwenye mitandao ya kijamii wakati yeye na wabunge wengine wakitembea kuelekea makazi ya Waziri Mkuu huko New Delhi.
Vuguvugu la maandamano ya Wahindi lnalojulikana kama “chama cha mende” iliapa Jumanne kuendelea na uhamasishaji wake hadi Waziri wa Elimu Dharmendra Pradhan ajiuzulu na mitihani ifanyiwe mageuzi.
Chama hicho, ambacho herufi zake za kwanza za CJP zinafanana na zile za Chama cha Bharatiya Janata cha Narendra Modi (BJP), kilianzishwa mwezi Mei na kinajivunia mamilioni ya wafuasi kwenye mitandao ya kijamii.
“Hatutaacha. Bw. (Dharmendra) Pradhan lazima afukuzwe kazi,” alisema Ashutosh Ranka, afisa wa chama, katika ujumbe uliochapishwa kwenye mitandao ya kijamii siku moja baada ya maandamano makubwa zaidi katika mji mkuu wa India katika kipindi cha miaka mitano.